Facebook

Tuesday, 10 June 2014

Mchekeshaji Tracy Morgan apata ajali mbaya ya gari.

tracy 
Mchekeshaji maarufu wa nchini Marekani Tracy Morgan bado yupo katika hali mbaya kiafya kutokana na ajali mbaya ya gari aliyopata mwishoni mwa wiki.
Muigizaji huyo wa vichekesho anakabiliwa na majeraha ya kuvunjika mbavu, pua na mguu baada ya gari aliyokuwa akisafiria kugongwa na gari kubwa na kusababisha ajali mbaya.
tracy2 
Baada ya kufanyiwa upasuaji wa mguu wake, Morgan ameanza kuonyesha matumaini lakini ataendelea kubaki hospitalini kwa wiki kadhaa akipatiwa matibabu, kwa mujibu wa msemaji wake.
Katika ajali hiyo iliyotokea mjini New Jersey muigizaji mwingine wa vichekesho Jimmy Mack, alipoteza maisha.


Tuko katika maboresho hivi karibuni blog hii itakuwa ni site ambayo itaitwa www.bantutz.com ni katika hatua za kuboresha huduma zetu za kutoa habari na burudani.Tutakuja katika muonekano mpya na bora zaidi.Vitu vizuri vipya usivyotarajia utaviona na kufurahia kupitia www.bantutz.com....


Related Posts:

0 comments:

Post a Comment