Mchekeshaji
maarufu wa nchini Marekani Tracy Morgan bado yupo katika hali mbaya
kiafya kutokana na ajali mbaya ya gari aliyopata mwishoni mwa wiki.
Muigizaji huyo wa vichekesho anakabiliwa na majeraha ya kuvunjika
mbavu, pua na mguu baada ya gari aliyokuwa akisafiria kugongwa na gari
kubwa na kusababisha ajali mbaya.
Baada ya kufanyiwa upasuaji wa mguu wake, Morgan ameanza kuonyesha matumaini lakini ataendelea kubaki hospitalini kwa wiki kadhaa akipatiwa matibabu, kwa mujibu wa msemaji wake.
Katika ajali hiyo iliyotokea mjini New Jersey muigizaji mwingine wa vichekesho Jimmy Mack, alipoteza maisha.
Tuko katika maboresho hivi karibuni
blog hii itakuwa ni site ambayo itaitwa www.bantutz.com ni katika hatua za
kuboresha huduma zetu za kutoa habari na burudani.Tutakuja katika muonekano
mpya na bora zaidi.Vitu vizuri vipya usivyotarajia utaviona na kufurahia
kupitia www.bantutz.com....
0 comments:
Post a Comment