Facebook

Monday, 2 June 2014

Ommy Dimpoz amefunguka kapata mchumba kupitia mitandao ya kijamii

 

Ommy amekiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM kuwa yeye na msichana huyo waliweza kukaa kwa muda wa mwaka mmoja wakichati bila kuonana.

“Social network zilisaidia kutuunganisha lakini matokeo yake mpaka tukaja kuonana. Mpaka nikaja kwenye tour tukaonana, si unajua kuna zile mzee unashangaa ma Instagram mtoto ka like picha kama tisini hivi, halafu ukichekecha unaona mbona kama umechorwaee ,bahati nzuri ilipoanzishwa instamessage kwa hiyo kama unajiiba hivi. Ni Mtanzania, mpaka kuonana ilichukua kama mwaka, tumechat tumechat mpaka ikafikia time, sina haraka kwanini niwe na haraka, kufahamiana kunakuja automatically,” alisema.

“Unajua mambo ya mapenzi Mungu mwenyewe ndio anajua, pengine wengine anaweza wewe ukawa muuza mkaa demu akaja kununua mkaa. Lakini lile kopo unavyolishika kimachejo wakati wa kupima yeye anapenda ule upimaji wako, kwahiyo kuna kitu kama hivyo haijalisha mnakutana wapi, ikiwa tu mmewekea mipaka yenu, masharti hivi na hivi maisha yenu yanaenda.
 
Endelea kutembelea katemimethsela.blogspot.com uweze kupata skendo na tetsi mbalimbali zinazowahusu wasanii.

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment