Facebook

Thursday, 12 June 2014

Ulaya wataka Blatter ajiuzulu kwa usemi

Rais wa Shirikisho la kandanda duniani, FIFA, Sepp Blatter.
Maafisa wa kandanda wa Europa sasa wamemtaka rais wa shirikisho la kimataifa la kandanda FIFA, Sepp Blatter, ajuzulu kutokana na madai ya rushwa yanayoindama Fifa.
Wametilia shaka uongozi wake.
Mkuu wa chama cha soka cha uholanzi Michael Van Praag, amesema chini ya uongozi wa Blatter ,Fifa imeandamwa na tuhuma za rushwa na ili Fifa kujisafisha ni sharti Blatter angatuke.
Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha soka Uingereza , Greg Dyke,amesthtumu kauli ya Blatter kuwa madai ya rushwa kuhusiana na kuchaguliwa kwa Qatar kuwa mwenyeji wa kombe la dunia 2022 yanayoripotiwa katika magazeti ya Uingereza yamechochewa na ubaguzi wa rangi.
Blatter anatarajiwa kutangaza nia yake ya kuwania nafasi kipindi cha tano kuingoza Fifa katika uchaguzi wa Fifa unaotarajiwa kufanyika mwaka ujao.
Kwa sasa wajumbe wa Fifa wanavikao huko Sao Paulo wakijiandaa kwa ufunguzi wa kombe la dunia hapo kesho ambako Sepp Blatter pia amekuwa akitoa cheche za maneno dhidi ya wale wanaoisema vibaya Fifa na Qatar.
 

Tuko katika maboresho hivi karibuni blog hii itakuwa ni site ambayo itaitwa www.bantutz.com ni katika hatua za kuboresha huduma zetu za kutoa habari na burudani.Tutakuja katika muonekano mpya na bora zaidi.Vitu vizuri vipya usivyotarajia utaviona na kufurahia kupitia www.bantutz.com....

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment