Facebook

Sunday, 8 June 2014

Yule mganga wa Ghana aendelea kumtengeneza Cristiano Ronaldo!

Maneno ya mganga wa kienyeji wa Ghana, Nana Kwaku Bonsam, yameanza kudhihirika baada ya uongozi wa timu ya taifa ya Ureno kuthibitisha taarifa za mshambuliaji Cristiano Ronaldo, kutokuwa sehemu ya kikosi cha timu ya taifa ya Ureno ambacho juzi kilicheza mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Mexico.

Nana Kwaku Bonsam, amesema yeye ndiye anayemroga nahodha huyo wa timu ya taifa ya Ureno, ili asicheze mchezo wa kundi la saba katika fainali za kombe la dunia ambapo timu ya taifa ya Ureno itapambana na timu ya taifa ya Ghana, Black Stars. 


Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Ureno Paul Bento alisema pamoja na kutarajia kumkosa Ronaldo katika mchezo wa juzi  wa kirafiki, bado hajafahamu ni lini mshambuliaji huyo atakuwa fit kwa ajili ya kujiunga na wenzake. 


Mshambuliaji huyo wa klabu ya Real Madrid anasumbuliwa na maumivu ya mishipa fulani laini katika mguu wake, ambapo kwa mara ya mwisho alionekana uwanjani wakati wa mchezo wa hatua ya fainali ya ligi ya mabingwa barani Ulaya walipocheza dhidi ya Atletico Madrid.




Tuko katika maboresho hivi karibuni blog hii itakuwa ni site ambayo itaitwa www.bantutz.com ni katika hatua za kuboresha huduma zetu za kutoa habari na burudani.Tutakuja katika muonekano mpya na bora zaidi.Vitu vizuri vipya usivyotarajia utaviona na kufurahia kupitia www.bantutz.com....

Related Posts:

  • Brazil kuchuana na Chile raundi ya pili Brazil ilitamatisha mechi za kundi kwa kishindo iliilaza Cameroon 4-1 Neymar alifunga mara mbili katika mechi aliyokuwa mchezaji bora wak… Read More
  • SUAREZ ADAIWA KUMNG'ATA MCHEZAJI TENA Picha za video zimeonesha mshambuliaji wa Uruguay Luis Suarez akimng'ata beki wa Italy Giorgio Chiellini. Mwamuzi hakuona kitendo hicho lakini huenda hatua zitachukuliwa baadaye. … Read More
  • Suarez apewa adhabu kali na FIFA STRAIKA wa Uruguay Luis Suarez amefungiwa Miezi Minne kutoshiriki chochote kwenye Soka baada ya kupatikana hatia ya kumuuma Meno Beki wa Italy Giorgio Chiellini. Straika huyo wa Liverpool pia amefungiwa Mechi 9 za Kimata… Read More
  • Uholanzi kumenyana na Mexico Uholanzi kuvaana na Mexico mkondo wa pili Uholanzi ilimaliza katika nafasi ya kwanza kwenye kundi B kufuatia ushindi wa mabao 2-0 katika mechi yao ya mwisho ya makundi. Mabao ya Uholanzi yaliyofungwa na Leroy Fern na… Read More
  • Van Gaal: ''FIFA imetuonea'' Van Gaal akashifu FIFA kwa ratiba mbaya za mkondo wa pili Kocha wa Uholanzi Louis van Gaal amelishutumu shirikisho la soka duniani FIFA kwa "kufanya hila" kwa jinsi linavyopanga ratiba ya michuano ya Kombe la Dunia… Read More

0 comments:

Post a Comment