Vyombo vya habari vya Nigeria vimeripoti habari ya mtu mmoja aliyekutwa
amefia kaburini kwamba alikubwa na umauti wakati akifanya jaribio la
kufukua kaburi ili aibe fuvu la marehemu kwa ajili ya matumizi ya mambo
ya kishirikina.
Kwa mujibu wa Saturday Tribune la Nigeria, tukio hilo limetokea katika
mji wa Ilobu eneo oa Osun ambapo mtu huyo alikutwa akiwa amekufa huku
nusu ya mwili wake ukiwa umeingia kaburini.
Mmoja wa wakazi wa eneo hilo ameeleza kuwa kijana huyo alikuwa na
marafiki zake wengine waliokuwa wanafanya tukio hilo kwa lakini baada ya
kuona mwenzao amenaswa ndani ya kaburi wakakimbia na kumuacha huku wao
wakiwa salama.
“Mwili wake ulikutwa majira ya saa kumi na mbili na nusu asubuhi na
kichwa chake kilikuwa kimefunikwa na tope. Wakazi wa eneo hili
waliripoti polisi na walikuja baadae wakautoa mwili wake na kuuweka
kwenye gari lao na kuondoka nae.” Alisema mkazi wa eneo hilo.
Saturday Tribune iliongea na kamishina wa Jeshi la Polisi wa eneo la
Osun, Ibrahi Maishanu ambaye alieleza kuwa polisi watafanya uchunguzi wa
kina kufuatia tukio hilo kufahamu nini hasa kilikuwa chanzo cha kifo
chake. Na kwamba polisi hawajathibisha kuwa tukio hilo linatokana na
masuala ya kishirikina
Endelea kutembelea katemimethsela.blogspot.com uweze kujua matukio mbalimbali yanayotokea duniani
Monday, 19 May 2014
Afia Kaburini Baada ya Kunaswa na Kitu Akijaribu Kufukua ili Aibe Fuvu
Related Posts:
Lowassa aitikisa Bariadi. Siku ya leo Mgombea Urais kupitia tiketi ya CHADEMA, Mh.Edward Ngoyai Lowassa alikuwa katika mji wa Bariadi na kujaza Umati mkubwa. Mh.Lowassa amejimadi kuimarisha huduma za jamii kama elimu, afya, maji na makazi. … Read More
Lowassa aahidi kuweka kipaumbele katika utoaji wa Elimu ya Kilimo.Mgombea urais wa vyama vinavyounda UKAWA Mh Edwad Lowassa amesema akichaguliwa kuwa Rais atahakikisha kuwa kipaumbele cha elimu pia kinatolewa kwa wakulima wafugaji na makundi mengine hatua itakayowawezesha kutekeleza majukum… Read More
Viongozi NCCR MAGEUZI wajitokeza kuelezea kutoridhishwa kwao na mwenendo wa UKAWAKatibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi Mosena Nyambabe azungumza juu ya Chadema kuteka Umoja wa UKAWA na kufanya ubabe katika katika upataji wa majimbo na kuacha vyama vingine vilivyo katika Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) leo… Read More
Mitambo ya kuzalisha Umeme wa gesi yawashwa rasmi Tanzania.Mkurugenzi mtendaji wa shirika la umeme nchini injinia Felchesmi Mramba amesema jana wamewasha rasmi mitambo ya kuzalisha umeme wa gesi iliyopo Ubungo jijini Dar es Salaam. … Read More
Jengo refu Afrika lazinduliwa Tanzania. Jengo la PSPF Towers lililozinduliwa na Rais Kikwete hapo jana ni moja ya majengo machache marefu barani Afrika na ndiyo jengo refu zaidi LILILOKAMILIKA Afrika Mashariki na Kati, likiwa na urefu wa mita 147. Ujenzi wake u… Read More
0 comments:
Post a Comment