Vyombo vya habari vya Nigeria vimeripoti habari ya mtu mmoja aliyekutwa
amefia kaburini kwamba alikubwa na umauti wakati akifanya jaribio la
kufukua kaburi ili aibe fuvu la marehemu kwa ajili ya matumizi ya mambo
ya kishirikina.
Kwa mujibu wa Saturday Tribune la Nigeria, tukio hilo limetokea katika
mji wa Ilobu eneo oa Osun ambapo mtu huyo alikutwa akiwa amekufa huku
nusu ya mwili wake ukiwa umeingia kaburini.
Mmoja wa wakazi wa eneo hilo ameeleza kuwa kijana huyo alikuwa na
marafiki zake wengine waliokuwa wanafanya tukio hilo kwa lakini baada ya
kuona mwenzao amenaswa ndani ya kaburi wakakimbia na kumuacha huku wao
wakiwa salama.
“Mwili wake ulikutwa majira ya saa kumi na mbili na nusu asubuhi na
kichwa chake kilikuwa kimefunikwa na tope. Wakazi wa eneo hili
waliripoti polisi na walikuja baadae wakautoa mwili wake na kuuweka
kwenye gari lao na kuondoka nae.” Alisema mkazi wa eneo hilo.
Saturday Tribune iliongea na kamishina wa Jeshi la Polisi wa eneo la
Osun, Ibrahi Maishanu ambaye alieleza kuwa polisi watafanya uchunguzi wa
kina kufuatia tukio hilo kufahamu nini hasa kilikuwa chanzo cha kifo
chake. Na kwamba polisi hawajathibisha kuwa tukio hilo linatokana na
masuala ya kishirikina
Endelea kutembelea katemimethsela.blogspot.com uweze kujua matukio mbalimbali yanayotokea duniani
Monday, 19 May 2014
Afia Kaburini Baada ya Kunaswa na Kitu Akijaribu Kufukua ili Aibe Fuvu
Related Posts:
BantuTz MAGAZETINI:Soma kilichoandikwa katika kurasa za magazeti yote ya leo Jumapili,Mei 31 MAGAZETINI-Ni uratatibu ambao BantuTz imeuanzisha ili kuwawezesha wadau wote wa Bantu waweze kusomana kupitia kurasa za magazeti mbalimbali nchini kila siku asubuhi ili kuwasogezea karibu zaidi huduma kupata habari nuhimu… Read More
BantuTz MAGAZETINI:Soma kilichoandikwa katika kurasa za magazeti yote ya leo Jumatatu,Juni 1. MAGAZETINI-Ni uratatibu ambao BantuTz imeuanzisha ili kuwawezesha wadau wote wa Bantu waweze kusomana kupitia kurasa za magazeti mbalimbali nchini kila siku asubuhi ili kuwasogezea karibu zaidi huduma kupata habari nuh… Read More
Hotuba ya Mh.Edward Lowassa akitangaza nia kugombea Urais kupitia CCMHOTUBA YA MHESHIMIWA EDWARD LOWASSA KWENYE MKUTANO NA WAANDISHI WA HABARI KWA AJILI YA KUTANGAZA NIA YA KUOMBA KUTEULIWA KUWA MGOMBEA WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) KWA NAFASI YA URAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA UTANGUL… Read More
BantuTz MAGAZETINI:Soma kilichoandikwa katika magazeti yote ya leo Jumanne,Juni 2. MAGAZETINI-Ni uratatibu ambao BantuTz imeuanzisha ili kuwawezesha wadau wote wa Bantu waweze kusomana kupitia kurasa za magazeti mbalimbali nchini kila siku asubuhi ili kuwasogezea karibu zaidi huduma kupata habari nuhimu… Read More
Wanachuo wapindua Serikali yao UDOM.Wanafunzi wa kitivo cha elimu katika chuo kikuu cha Dodoma wameipindua serikali ya wanafunzi wa kitivo hicho kwa madai ya kutowajibika kwa viongozi pamoja na madai ya ubadhirifu wa fedha. Chuo Kikuu cha Dodoma(UDOM). Mapinduz… Read More
0 comments:
Post a Comment