Vyombo vya habari vya Nigeria vimeripoti habari ya mtu mmoja aliyekutwa
amefia kaburini kwamba alikubwa na umauti wakati akifanya jaribio la
kufukua kaburi ili aibe fuvu la marehemu kwa ajili ya matumizi ya mambo
ya kishirikina.
Kwa mujibu wa Saturday Tribune la Nigeria, tukio hilo limetokea katika
mji wa Ilobu eneo oa Osun ambapo mtu huyo alikutwa akiwa amekufa huku
nusu ya mwili wake ukiwa umeingia kaburini.
Mmoja wa wakazi wa eneo hilo ameeleza kuwa kijana huyo alikuwa na
marafiki zake wengine waliokuwa wanafanya tukio hilo kwa lakini baada ya
kuona mwenzao amenaswa ndani ya kaburi wakakimbia na kumuacha huku wao
wakiwa salama.
“Mwili wake ulikutwa majira ya saa kumi na mbili na nusu asubuhi na
kichwa chake kilikuwa kimefunikwa na tope. Wakazi wa eneo hili
waliripoti polisi na walikuja baadae wakautoa mwili wake na kuuweka
kwenye gari lao na kuondoka nae.” Alisema mkazi wa eneo hilo.
Saturday Tribune iliongea na kamishina wa Jeshi la Polisi wa eneo la
Osun, Ibrahi Maishanu ambaye alieleza kuwa polisi watafanya uchunguzi wa
kina kufuatia tukio hilo kufahamu nini hasa kilikuwa chanzo cha kifo
chake. Na kwamba polisi hawajathibisha kuwa tukio hilo linatokana na
masuala ya kishirikina
Endelea kutembelea katemimethsela.blogspot.com uweze kujua matukio mbalimbali yanayotokea duniani
Monday, 19 May 2014
Afia Kaburini Baada ya Kunaswa na Kitu Akijaribu Kufukua ili Aibe Fuvu
Related Posts:
Upinzani Watoa Tamko lao leo kuhusu kugomea Vikao Vya Bunge....soma soma kauli zao mbalimbali hapa...... Baada ya kugoma na kuamua kutoka nje ya bunge la katiba Dodoma kikundi cha umoja wa katiba ya Wananchi (UKAWA) kimekutana na waandishi wa habari April 17 2014 na kuyazungumza haya yanayofata hapa chini… Read More
Sababu za Upinzani Jana kususia kikao cha bunge hizi hapa...... Leo katika kipindi cha Kumepambaz kinachorushwa hewani na kituo cha Radio cha RADIO ONE STERIO alisikia Kamanda Aikael Freeman Mbowe akitoa ufafanuzi wa UKAWA kutoka nje ya bunge maalumu la katiba na kutorudi tena b… Read More
Angalia katika Picha Namna Wajumbe wa Bunge La Katiba Kutoka Upinzani Walivyogoma Na kutoka Nje Ya ukumbi wa Bunge Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba ambao wanaunga mkono mfumo wa Serikali za tatu wakitoa katika Ukumbi wa Bunge leo mjini Dodoma baada ya kususia kikao Wajumbe wa Bung… Read More
Msichana aliyeteswa kinyama kwa miaka 9 aokolewa.......fuatilia hapa... Polisi nchini Argentina wamemwokoa msichana mwenye umri wa miaka kumi na mitano ambaye alifungiwa katika chumba cha kuegesha magari na kunyimwa chakula pamoja na kupigwa na wazazi waliokuwa wamemuasili, kwa kipin… Read More
Rais Kikwete akerwa na Wanasiasa kumtukana Mwalimu J.K.Nyerere...soma hapa barua aliyoiandika.......... Rais Kikwete akerwa na kitendo cha wanasiasa kumtukana muasisi wa Taifa hili Mwalimu Nyerere....Asema ni utovu wa nidhamu kuwatukana waasisi wa Tanzania hususan Mwalimu J.K Nyerere na Sheikh Abeid Aman Ku… Read More
0 comments:
Post a Comment