Facebook

Wednesday 14 May 2014

Hivi ndivyo Siasa ilivyozima ndoto za Marlaw



Akiwa kijana mdogo ambae alianzia shughuli zake za mziki mji mdogo
unaoitwa MASWA huko SHINYANGA Marlaw alikua na ndoto za kua msanii mkubwa kama kina R. Kelly,Usher Raymond na wengine kwani sauti yake ilikua na uwezo mkubwa na alikua anaweza copy na kupaste kila kitu cha R. kelly.


Ndoto hizo zilimwagiliwa na kuchipuka pale aliposhinda mashindano ya Coca Cola Pop Star na kwenda kuwakilisha kanda ya Ziwa Jijini Nairobi ambako aliibuka katika Tano bora.




Aliporudi Tanzania aliendelea na masomo baada ya kumaliza kidato cha nne aliendelea na masomo ya juu yaani form 5 na 6 huko Mtwango sec Iringa baada ya jitihada za kujiunga Makongo kugonga mwamba.

Huko ndipo alikutana na Tuddy Thomas aliekua akitengeneza mziki wake katika mji wa Iringa na wakafanikiwa kurekodi nyimbo ambazo zilimweka Marlaw kwenye ramani ya mziki wa Bongo Flava.


Alifanikiwa kuteka vilivyo soko la mziki ndani na hata nje ya nchi na kufanikiwa kufanya show nyingi kuliko msanii yeyote kipindi hicho (2004/2005).



Nyimbo zake ziliendelea kushika chart mabali mbali mpaka nje ya nchi na mda flani zilitumika hata katika hafla za kisiasa.

Mnamo mwaka 2005 kipindi cha uchaguzi Marlaw alilipwa takribani 100,000,000 Million za kitanzania ili kukipingia kampeni chama kikubwa cha siasa hapa Tanzania (CCM) na kilifanikiwa kushinda kwa kishindo


Endelea kutembelea katemimethsela.blogspot.com uweze kujua taarifa mbalimbali zinazowahusu wasanii ambazo hautazisikia sehemu nyingine

0 comments:

Post a Comment