Facebook

Monday, 5 May 2014

Unazijia sababu zilizomfanya Jaguar kutohudhuria tuzo za KTMA.....?? hizi hapa.....


Screen Shot 2014-05-05 at 5.58.39 PM 

Staa wa muziki wa Kenya anaetajwa kuingia kwenye TOP 5 ya Wasanii matajiri wa muziki wa kizazi kipya Afrika Mashariki huku orodha hiyo ikiwa na watu wengine kama Jose Chameleone.
Imefahamika kwamba Jaguar alikataa kuja kwenye tuzo za Kili 2014 alizokua nominated baada ya waandaaji kushindwa kufikia masharti aliyowapa na badala yake akaamua kwenda kuhudhuria harusi ya producer wa DNA aitwae Refigah.
Jaguar alitaka atumiwe ticket ya ndege ya business class, alitaka achukuliwe chumba kwenye hoteli ya nyota tano, apewe ulinzi popote atakapokwenda na vilevile apewe gari zuri la kifahari la kutembelea.
Kwenye sharti jingine Jaguar alitoa option kwa waandaaji na kuwaambia kama wangeshindwa kumpa ticket ya ndege basi walipaswa kuweka mafuta ili aje na ndege yake ndogo anayomiliki.
Chameleone, Wyre, Amani, Ay, Mtangazaji William Tuva, shabiki Daudi wa Kota na friends juzi Dar es salaam.
Chameleone, Wyre, Amani, Ay, Mtangazaji William Tuva, shabiki Daudi wa Kota na Dj wa Chameleone juzi Dar es salaam.
Alipohojiwa na ghafla.co.ke Jaguar alisema asingeweza kuhudhuria tukio ambalo asingepewa heshima aliyoitaka kama ambavyo huwa anaipata anapokwenda kwenye nchi nyingine katika matukio kama haya ndio maana ilikua bora ahudhurie harusi na kuongeza kwamba ‘nitahudhuria iwapo wataanza kuwa-treat vizuri wasanii wa Kenya’
Tuzo za KILI 2014 zilihudhuriwa na mastaa wawili wa Kenya ambao ni Wyre na Amani huku Uganda ikiwakilishwa na Jose Chameleone ambae ndio alitangazwa mshindi kwenye kipengele cha Afrika Mashariki.

Endelea kutembelea katemimethsela.blogspot.com kupata habari mbalimbali kwa muda muafaka.....

Related Posts:

  • Mahakama:Pistorius hakukusudia kuuaJaji anayetoa uamuzi katika kesi ya mauaji inayomkabili Oscar Pistorius, amesema upande wa mashitaka umekosa kuthibitishia kikamilifu shitaka kuu la kwanza dhidi ya Pistorius kuwa alikusudia kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp… Read More
  • Oscar hatiani kwa kuua bila kukusudiaMwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini Oscar Pistorius, amepatikana na hatia ya kumuua mpenziwe Reeva Steenkamp kwa bahati mbaya Akitoa uamuzi wake jaji Thokozile Masipaal alisema kuwa mwanariadha huyo alimuua Reeva kwa bahati … Read More
  • Mtanzania ateuliwa kuwa makamu mkuu wa Rais wa BET Networks.  BET Networks, ambayo ipo chini ya kampuni ya Viacom Inc. imetangaza kumwajiri Kay Madati kama makamu mkuu wa rais (Executive Vice President) na pia kama Chief Digital Officer. Madati, raia wa Tanzania aliyeishi katik… Read More
  • Clouds kulishitaki gazeti la Aman kwa kumchafua Diva.Kampuni ya Clouds Media Group yenye makao makuu jijini Dar Es Salaam inataka kulishitaki gazeti la Aman kwa kumchafua mmoja wa watangazaji wake mahiri Loveness Malinzi alimaarufu kama "Diva Loveness";mtoto wa Rais wa Shirikis… Read More
  • Q Chilla alamba dili nonoMsanii wa muziki wa Bongofleva Abubakari Katwila almaarufu kama Q Chief amevunja ukimya kwa kupata dili la mkataba wa mamilioni na kampuni ambayo itakuwa ikisimamia kazi zake za muziki zitakazotengenezwa kwa ubora wa hali ya … Read More

0 comments:

Post a Comment