
Waandamanaji wakipambana na polisi Uturuki siku ya Wafanyakazi
Maandamano na vurugu zimefanyika
leo siku ya siku ya wafanyakazi duniani katika mji mkuu wa Uturuki wa
Istanbul na maeneo mengine duniani.
Maafisa wa polisi walitumia mabomu ya kutoa
machozi pamoja na maji baada ya waandamanaji kukaidi marufuku ya
kuandamana katika bustani Taksim.
Wandamanaji wakiwatupia polisi fataki

Waandamanaji wakijikinga na vifaa vya kuzuia madhara ya mabomu ya machozi

Medani ya Taksim Square
Serikali ya Uturuki imewapeleka mamia ya maelfu ya maafisawa polisi pamoja na kusimamisha usafiri wa umma.
Waziri Mkuu Recep Tayyip Erdogan mapema aliwaonya watu walikuwa na matumaini ya kukusanyika kwenye medani ya Taksim kuwa itaonyesha ni hatua ya kuipinga serikali.
Nako nchini Cambodia ,watu kadhaa wamedaiwa kupigwa na polisi wanaolinda usalama walipojaribu kuvuruga maandamano ya wapinzani waliokuwa wakiandamana katika mji mkuu wa Phnom Penh.
0 comments:
Post a Comment