Facebook

Thursday, 12 June 2014

Malawi waanza chokochoko ndege yao yaonekana Ileje

MBUNGE wa Ileje, Aliko Kibona (CCM) ameomba Serikali ieleze juu ya ndege kutoka Malawi, ambayo imekuwa ikitia hofu wananchi wa Ileje, kwa kuzunguka angani kila mara.

Mbunge huyo alisimama kutoa hoja hiyo baada ya kipindi cha maswali na majibu na kuomba mwongozo wa Spika, Anne Makinda kuhusu suala hilo. Kibona alisema:

“Nazungumzia jambo mahsusi linalotokea katika mpaka wa Tanzania na Malawi katika Jimbo la Ileje. Kwa sasa kuna ndege kutoka nchi ya Malawi inazunguka katika vijiji jirani na tayari imeleta hofu kwa wananchi; na watoto hawawezi kusoma. Ninaomba mwongozo wako kama nipo sahihi. Naitaka Serikali kwanza ieleze ile ndege inatoka wapi na inafanya nini; na Pili naitaka Serikali imfahamishe Mkuu wa Wilaya ya Ileje kuhusu ndege hiyo ili naye awafahamishe wananchi ili wasiwe na hofu”.

Mbunge huyo alisema aliamua kuleta hoja hiyo bungeni, kwa kuzingatia uhusiano uliopo hivi sasa baina ya Tanzania na Malawi. Baada ya maelezo hayo ya Kibona, Spika alisema:

“Suala la Mheshimiwa Kibona linahitaji kufanyiwa kazi sana”. Serikali inaendelea na vikao vyake na itampatia majibu Kibona baada ya kutafakari na kujadili suala hilo.
 
Tuko katika maboresho hivi karibuni blog hii itakuwa ni site ambayo itaitwa www.bantutz.com ni katika hatua za kuboresha huduma zetu za kutoa habari na burudani.Tutakuja katika muonekano mpya na bora zaidi.Vitu vizuri vipya usivyotarajia utaviona na kufurahia kupitia www.bantutz.com....
 

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment