Facebook

Saturday, 7 June 2014

Mtoto mchanga auwawa kwa kufungwa Plasta mdomoni na puani kisha kutupwa.

Mtoto mchanga, amekutwa ametupwa pembezoni mwa barabara ya Kawe-Beach, huku puani na mdomoni akiwa amefungwa plasta, iliyosababisha kukosa pumzi na kufariki.

Katika hali isiyo ya kawaida mwanamke mmoja ambaye hakujulikana jina lake wala kujua anapoishi, anasadikika kutenda ukatili na unyama wa hali juu kwa kumuua huyo mwanaye na kisha kumtupa pembezoni mwa barabara hiyo.

Wavuvi wa eneo hilo waliona mfuko pembezoni ukiwa na damu hali ambayo iliwashtua na kuamua kusogea karibu, ndipo walipomkuta mtoto huyo mwenye jinsi ya kike, akiwa amefariki huku akiwa amefungwa plasta mdomoni na puani.
 
 
Tuko katika maboresho hivi karibuni blog hii itakuwa ni site ambayo itaitwa www.bantutz.com ni katika hatua za kuboresha huduma zetu za kutoa habari na burudani.Tutakuja katika muonekano mpya na bora zaidi.Vitu vizuri vipya usivyotarajia utaviona na kufurahia kupitia www.bantutz.com....

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment