Facebook

Tuesday 13 May 2014

MAPATO KWA VILABU LIGI KUU UINGEREZA MSIMU 2013-14


Klabu zina njia kuu 3 za kujipatia kipato:-
1. mapato ya mechi - viingilio, kuuza chakula na vinywaji na nk
2. mapato ya kibiashara - shati wazamini, mikataba ya vifaa mbalimbali, bidhaa
3. mapato vyombo vya habari - televisheni na vingine vinavyohusika ( FA wanahusika zaidi)

Wanaoshiriki uefa champions na europa league wanapata zaidi, timu zilizopata nafasi za kushiriki uefa champions league ana uhakika wa kupata paundi milioni 25 kutoka chama cha ulaya kwa kushiriki tu hatua ya makundi.
kutokana na mkataba mnono wa televisheni waliopata FA kwa ajili ya ligi ya 2013-14 mapato ya vilabu yamepanda maradufu.
Mapato ya televisheni ugawiwa kwa usawa kama mchanganuo ufuatao:-
1. kiasi cha paundi 1.2milini kwa nafasi = bingwa 1.2x20 na wa mwisho anapata hiyo 1.2milioni ( msimu uliopita ilikuwa paundi 750,000)
2. idadi ya mechi zilizooneshwa mara paundi 750,000
3. gawiwo la televisheni ambapo utolewa sawa kwa timu zote, msimu huu paundi milioni 55.

Kipengele hiki cha kugawana mapato ya uwiano mzuri ndio kinachoifanya ligi ya uingereza kuwa na ushindani mzuri, sababu walau timu zote zina uwezo wa kusajili na kujiendesha.
Kupanda kwa mapato msimu huu jumlisha na mfumo mzuri wa kugawana mapato unapelekea kuona Manchester United paundi milioni 60.8 ni kidogo ukilinganisha na kiasi ambapo anapata timu iliyoshika nafasi ya mwisho katika ligi, Cardiff City.
Ukiangalia njia ya 3 ya mapato ya klabu, Liverpool FC itajinyakulia fedha nyingi kutoka FA kuliko bingwa sababu mechi zake nyingi zimerushwa kuliko Manchester City. LFC mechi 28 na bingwa zimerushwa mechi 25.
Na katika hilo wamiliki wa Liverpool FC wamshukuru Brendan Rodgers kwa kumpatia mkataba mnono sababu ya mfumo wa mpira alioleta ikichagizwa na aina ya wachezaji aliotumia. Waandishi na watangazaji waliita Liverpool FC Free Flowing Football, Free Flowing Goals ilisababisha watu kupenda kuangalia mechi za Liverpool zaidi.
Msimamo wa mechi zilizorushwa LIVE
Liverpool FC mechi 28
Manchester City mechi 25
Manchester Utd mechi 25
Arsenal FC mechi 25
Chelsea FC mechi 24
Tottenham mechi 23

Bingwa kapata paundi milioni 97.7
Liverpool Fc paundi milioni 98.8

0 comments:

Post a Comment