Facebook

Monday 12 May 2014

Nisha aweka wazi sababu zilizomfanya aachane na Ney wa Mitego...

Msanii wa maigizo Salama Jabu maarafu kama Nisha amefunguka na kueleza sababu kubwa iliyomfanya kusitisha penzi lake na mwanabongo flava Nay wa Mitego. Akiongea  Nisha alisema" Unajua Nay ndiye mwanaume pekee aliyefanikiwa kuuteka mtima wangu hadi leo hii sipata mwanaume anaejua mapenzi kama yeye lakini sasa nilikuwa napata shida sana kwake" Alisema Nisha Msanii huyo aliendelea kusema kuwa
" Unajua Nay kwenye maapenzi ni balaa anajua sana yani sikuamini kama ningekuja kuachana nae lakini kutokana na mazingira ya yule mtu sikuwa na jinsi nikaamua kumpigia chini" Alisema Hata hivyo Nisha alizitaja sababu kubwa  zilizopelekea kuchukua uamuzi huo ni pamoja na ukorofi wa mwanamuziki huyo pamoja na matusi matusi ndiyo maana alichukua maamuzi hayo magumu

Endelea kutembelea katemimethsela.blogspot.com uweze kupata stori mbalimbali zinazowahusu mastaa

0 comments:

Post a Comment