Facebook

Tuesday 13 May 2014

Unakijua walichokisema Lulu na Dr.Cheni baada ya Dr.Cheni kuzushiwa kifo.....fuatilia hapa...



Mwigizaji na muongozaji wa bongomovie Dr. Cheni ambaye alianza kupata umaarufu kwenye fani ya uigizaji na thamthilia za kundi la Kaole na sasa akiwa anafanya movie zake, 12 May alizushiwa kifo ikiwa imeunganishwa na ishu yake ya kulazwa hospitali kutokana na homa ya dengu.
Baada ya huo uvumi kusambaa Elizabeth Michael ”Lulu” aliandika 

 ‘Jamani kuna mambo ya kuzushiana lakini sio kifo, kuna habari zimezushwa kwamba Dr. Cheni amefariki, ni habari za uongo jamani…. yuko salama kabisa na juzi ameruhusiwa kutoka hospital na anaendelea vizuri, tunajua kufa ni wajibu lakini mpaka Mungu mwenyewe apende….. pole baba angu’


Dr Cheni na yeye aliandika ‘Jamani kifo kipo na hakuna atakaekwepa ni lazima tutakufa na hakuna atakaebakia ila si vyema kunizushia, siku yangu itafika tu na wote mtajua lakini si jambo la busara kunizushia.
 
Endelea kutembelea katemimethsela.blogspot.com kupata habari mbalimbali zinazowahusu wasanii

0 comments:

Post a Comment