Facebook

Friday 9 May 2014

Ufisadi:Magari Mapya 11 Yaliyonunuliwa na Serekali Hayajulikani Yalipo


Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG imeamplfy kwamba kitendo cha Serikali kukosa nyaraka za mali zake kumechangia baadhi ya watendaji wasio waaminifu kutumia mwanya huo kujisogezea mali za umma.

Katika ripoti yake ya Ukaguzi kwa mwaka 2013 CAG Ludovick Utouh amesema ofisi yake imebaini upotevu wa magari 11 yaliyonunuliwa kwa ajili ya matumizi na mamlaka ya maendeleo na biashara Tanzania (TanTrade) ambayo hadi sasa hayafahamiki yalipo.
Ofisi yake inalifanyia uchunguzi suala hilo na tayari imegundua hayo magari yalisajiliwa kwa namba binafsi badala ya namba za serikali huku akisema ‘wizara ya viwanda na biashara ilinunua magari kwa ajili ya bodi ya biashara  na tunaomba kusema magari hayo tumejaribu kuyafatilia lakini hayaonekani na hayajulikani yalipo na ni magari mapya yalinunuliwa kwa ajili ya TanTrade lakini TanTrade wenyewe wanasema hawajayapokea na Wizara inasema haijui yako wapi’

0 comments:

Post a Comment