Mpira wa bara la Ulaya utakuwa na mabadiliko makubwa sana kama
ikitokea Lionel Messi anaondoka Barcelona, hii ni kauli ya kocha wa
Chelsea Jose Mourinho.
Messi amekuwa ni mtu muhimu sana katika klabu ya Barcelona kwa
takribani muongo mmoja sasa, akiwasaidia kutwaa makombe matatu
ya ligi ya mabingwa Ulaya, makombe saba ya La Liga na mengine
kadhaa ambayo hayajatajwa.
Mourinho, ambaye alimpoka taji la La Liga Guardiola mwaka 2012
wakati akiinoa Real Madrid anahisi kuwa Muargentina huyo mwenye
umri wa miaka 27 ndio nguzo kubwa ya mafanikio ya klabu hiyo
"Ndani ya kipindi cha miaka 10 ambacho Messi hatokuwepo, ramani
ya soka la Ulaya lazima itabadilika sana," Mourinho aliiambia
talkSPORT.
"Walichoshinda Barcelona katika miaka kadhaa iliyopita wakiwa ama
na Frank Rijkaard, Pep Guardiola au Luis Enrique kama makocha ni
kwa sababu wamekuwa na kiumbe huyu."
Chelsea wamewahi kuhusishwa na kumwania Messi, ambaye kwa
wakati fulani alionekana kutokuwa na furaha klabuni hapo, lakini
Mourinho alikanusha vikali taarifa hizo.
Pia Jose Mourinho amesisitiza kuwa Barcelona na Real Madrid
zingekutana na kibarua kigumu kushinda kombe la ligi kuu England.
Soka la Hispania halimridhishi Mourinho akidai halina ushindani licha
ya yeye kushinda kombe la La Liga kwa rekodi ya pointi mia moja na
magoli 121 mwaka 2012 akiwa kocha wa Real Madrid.
Chelsea wametawazwa mabingwa wa ligi kuu zikisalia mechi tatu,
lakini Mourinho anadai wamefikia mafanikio kwa kutoa jasho
kwasababu England hakuna vitu rahisi kama La Liga.
Mourinho amesisitiza kuwa alipokuwa Hispania hakuwa na furaha
kwasababu alitwaa ubingwa kwa rekodi ya pointi na magoli mengi,
lakini alicheza mechi nne au tatu kwa msimu mzima.
Pia alipoteza ubingwa kwa pointi 92 huku akicheza tena mechi nne au
tano kwa msimu mzima.
Tuesday, 19 May 2015
Mourinho "Soka la Ulaya litabadilika endapo Messi atahama Barcelona"
Related Posts:
RATIBA YA MECHI ZOTE ZA KOMBE LA DUNIA KWA MASAA YA AFRIKA MASHARIKI Hapa ni kwa masaa ya kawaida nyumbani east Africa....fahamu muda gani timu uipendayo itashuka dimbani Group AGroup BGroup CGroup DGroup EGroup FGroup GGroup H BrazilSpainColombiaUruguaySwitzerlan… Read More
Kinachojiri nchini Brazil kabla ya Kombe la dunia kuanza..! Ikiwa imebakia siku moja kabla ya michuano ya kombe la dunia ambayo ni mikubwa kabisa kwa upande wa soka ikiwa inayovutia mabilioni ya watazamaji duniani kuanza –www.bantutz.com itakuwa inakuletea yote yanayojiri nchini… Read More
Maajabu ya mmiliki wa klabu ya Southampton.. Katharina Liebherr: Jina hili la mama huyu kibonge si maarafu sana katika vichwa na midomo ya wapenda soka duniani hasa bongo,labda ni kwa sababu ya jinsia yake ama ni kutokana na tabia yake ya kujiweka mbali na vyomb… Read More
Sepp Blatter:Wabaguzi ndio wanapinga Qatar Rais wa shirikisho la kandanda duniani, FIFA, Sepp Blatter. Mkuu wa shirikisho la kandanda, FIFA, Sepp Blatter amesema madai ya rushwa katika uchaguzi wa Qatar kuwa mwenyeji wa kombe la dunia 2022 yamechochewa na hi… Read More
Hatimaye Cameroon waelekea Brazil Hatimaye The Indomitable Lions ya Cameroun waabiri ndege ya Brazil Cameroon sasa wameenda Brazil baada ya mzozo kuhusu marupurupu yao kutatuliwa. Wachezaji hao , almaarufu 'Indomitable Lions' walikuwa wamesusia kuing… Read More
0 comments:
Post a Comment