Facebook

Friday, 11 July 2014

Tetesi za usajili katika magazeti mbalimbali barani Ulaya.

TETESI ZA SOKA ULAYA
Salim Kikeke's photo.
Kocha mpya wa Manchester United Louis van Gaal angependa kumchukua Wesley Sneijder, 30, kutoka Galatasaray, lakini klabu hiyo ya Uturuki inataka pauni takriban milioni 6 (Sun),
 Salim Kikeke's photo.
 Liverpool watamuuza Luis Suarez, 27, kwenda Barcelona mwisho wa wiki hii, ikiwa klabu hizo zitakubaliana ada ya pauni milioni 75 (Daily Mirror), 
 
Lakini Arsenal wamekasirishwa kwa sababu jaribio lao la kumchukua Alexis Sanchez, 25, kutoka Barcelona linacheleweshwa kutokana na mkataba wa Suarez kudemadema (Daily Express), 
 
Arsenal wanataka kulipwa pauni milioni 6 kumuuza Mikel Arteta, 32, kwenda Fiorentina (Times), 
 
Roma wamewapa Manchester City hadi tarehe 21 mwezi huu wawe wamekamilisha usajili wa beki wa kati kutoka Morrocco Mehdi Benatia, 27, (Guardian), 
 Salim Kikeke's photo.
Chelsea wanamsajili beki wa kulia wa Atletico Madrid, Luis Filipe, 28, kuziba nafasi ya Ashley Cole aliyekwenda Roma (Sun), 
 
Winga kutoka Colombia Juan Cuadrado, 27, huenda akahamia Manchester United kutoka Fiorentina (London Evening Standard),
 
Mshambuliaji wa Liverpool Iago Aspas, 26, anajiandaa kuhamia Sevilla, baada ya kushindwa kupata namba Anfield (Daily Star), 
 
Brendan Rodgers pia anafikia kutoa pauni milioni 10 kumchukua beki wa kushoto wa Swansea Ben Davies, 21 (Daily Telegraph), 
 
Manchester United, Liverpool, Chelsea na Arsenal zitapambana kupata saini ya winga wa Benfica Joao Filipe anayetajwa kuwa "Cristiano Ronaldo mwingine" pamoja na kipa Joao Virginia, wote wana umri wa miaka 15 (Daily Express), 
 
Manchester United wanafikiria kumsajili beki wa kushoto wa Wolfsburg na Uswisi, Ricardo Rodriguez, 21, kuziba nafasi ya Patrice Evra ambaye huenda akahamia Juventus (Times), 
 
Lakini Louis van Gaal pia huenda akamchukua beki Daley Blind, 24, kutoka Feyenoord ikiwa Evra ataondoka (Manchester Evening News),
 
 kiungo kutoka Nigeria Michael Babatunde, 21, anayechezea Volyn Lutsk nchini Ukraine, amedai kuwa Sunderland wanataka kumsajili (Newcastle Chronicle), 
 Salim Kikeke's photo.
Bayern Munich wamesema wamefikia makubaliano yasiyo ya maandishi na Atletico Madrid ya kumsajili Mario Mandzukic, 28 (Marca),
 
 Mshambuliaji wa Real Madrid Alvaro Morata huenda akajiunga na Juventus mapema wiki ijayo (Tuttosport),
 
Hatimaye, kinyozi wa Alexis Sanchez amethibitisha kuwa mchezaji huyo anahamia Arsenal! (Metro).
 
 Share tetesi hizi na wapenzi wote wa soka. Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Cheers!

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment