Facebook

Friday, 5 September 2014

Matangazo tiba za asili yapigwa marufuku.


Matangazo ya tiba za asili yanaelezwa kupotosha uma
Baraza la Tiba za Asili na Tiba Mbadala Tanzania limesitisha vibali vya kurusha matangazo ya tiba za asili na mbadala kwenye vyombo vyote vya habari kwa kile kilichoelezwa kuwa yanapotosha jamii.
Taarifa iliyotolewa na kwa vyombo vya habari , imeeleza kuwa katika siku za karibuni kumekuwapo na matangazo mbalimbali ya tiba hizo ambayo baadhi yake hayaisaidii jamii.

Kutokana na taarifa hiyo ya baraza, vyombo vya habari havipaswi kupokea kibali chochote cha kutangaza matangazo ya tiba hizo hivi sasa, kwa kuwa ni batili.
Pia taarifa hiyo inaeleza kuwa, chombo chochote kitakachorusha tangazo au kipindi kitatozwa faini na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.
Naye mtaalam wa tiba asili, tabibu Rahabu Rubago amesema kuwa hatua hiyo ya Baraza imetolewa bila wao kupatiwa taarifa hiyo mapema na kueleza kuwa watapata hasara kwa kuwa baadhi yao wametengeneza vipindi tayari kwa ajili ya kuvirusha kwenye vyombo vya habari.

Related Posts:

  • Wanafunzi 12,000 wakosa nafasi Vyuo vikuu,TCU yawapa nafasi ya Pili.Wanafunzi 12, 000 wakosa nafasi za vyuo vikuu, TCU yawapa nafasi ya pili kuchagua nafasi za masomo (course) ambazo bado ziko wazi na wameshauriwa kutochagua "course" zenye ushindani mwingi maana hii itasababisha wengine kukos… Read More
  • Matangazo tiba za asili yapigwa marufuku. Matangazo ya tiba za asili yanaelezwa kupotosha uma Baraza la Tiba za Asili na Tiba Mbadala Tanzania limesitisha vibali vya kurusha matangazo ya tiba za asili na mbadala kwenye vyombo vyote vya habari kwa kile kili… Read More
  • MIFUPA YA DINOSARIA "GODZILLA" YAPATIKANA TANZANIAAina mpya ya dinosaria imetambuliwa kufuatia kupatikana kwa mifupa nchini Tanzania. Mabaki hayo ya dinosaria yaliyopewa jina la - Rukwatitan Bisepultus - yalipatikana katika korongo moja kwenye eneo la Rukwa, kusini magharibi… Read More
  • Nyangumi apatikana Mtwara.Mzoga wa samaki aina ya nyangumi Umepatikana katika pwani ya Bahari ya Hindi Mkoani Mtwara na kisha kuvutwa Kuelekea majini na wavuvi wa Kata ya Msangamkuu. Mzoga huo una urefu wa futi 48 na uzito unaokadiriwa kuwa zaidi ya t… Read More
  • Apple wazindua bidhaa mpya.Kampuni ya Apple imezindua saa ya kisasa - the Apple Watch - ambayo ni bidhaa yake mpya tangu iPad ya kwanza na tangu kifo cha mmoja wa waasisi wake Steve Jobs. Kifaa hicho huendesha programu tumishi (apps) na pia hufuatilia … Read More

0 comments:

Post a Comment