Kocha wa Costa Rica, Jorge Luiz Pinto ametoa maoni kuwa winga
machachari wa Kidachi Arjen Robben anastahili adhabu kali kama atajaribu
kurudia ile tabia yake ya kujiangusha ndani ya eneo la penati kama
alivyofanya kwenye mechi ya kuingia robo fainali dhidi ya Mexico.
Hatahivyo Robben mwenye miaka 30 aliomba msamaha katika vyombo vya
habari mara baada mechi kumalizika kwa ushindi wa 2-1 huku goli la
ushindi likifungwa mara baada ya mwamuzi wa mechi hiyo kutoa adhabu ya
penati huku akidhani Robben alikuwa amefanyiwa madhambi katika eneo la
penati na beki wa Mexico Rafael Marquez.
Pinto ambaye ndio kocha mkuu wa Costa Rica alisikika akisema kuwa,
amewaomba Fifa pamoja na mwamuzi wa mechi yao hiyo ya Jumamosi kumtupia
jicho la ziada winga huyo ili asije akaigharimu timu yao katika kuelekea
kwenye nusu fainali ya michuano hii ya Kombe la Dunia.
Costa Rica imefikia katika hatua ya robo fainali mara baada ya kuiondoa Ugiriki katika changamoto ya mikwajuu ya penati.
Mechi hiyo ya leo Jumamosi inatazamiwa kuanza saa 5 kamili usiku kwa
saa za Afrika Mashariki katika uwanja wa Arena Fonte Nova uliopo katika
Jiji la Salvador
Related Posts:
Jack Wilshare ashtakiwa na FA.
Kiungo wa Arsenal Jack Wilshere ameshtakiwa na chama cha soka cha
England, FA kufuatia tukio la kwenye msafara wa basi wakati wa
kusherekea ushindi wa Kombe la FA. Taarifa ya FA imesema:
"Inatuhumiwa kuwa tabia yake ya k… Read More
Diego Costa akanusha taarifa za kutaka kuondoka Chelsea.
Mshambuliaji
Diego Costa ametupilia mbali taarifa kuwa anataka kuondoka Chelsea na
kurejea Spain. Mchezaji huyo, 26, alihamia Chelsea akitokea Atletico
Madrid mwaka jana kwa pauni milioni 32.Akizungumza na Chelsea T… Read More
Berbatov afungashiwa virago Monaco.
MSHAMBULIAJI
wa zamani wa kimataifa waBulgaria, Dimitar Berbatov anatafuta timu ya
tatu ya kujiunganayo England, baada yakutemwa na AS Monacoya Ufaransa.
Berbatov alijiunga na vigogo hao wa Ligue 1 Januari mwaka 2014 ku… Read More
Tetesi zote za Usajili wa wachezaji barani Ulaya siku ya leo.Dau la Manchester United la
pauni milioni 110 kwa Real Madrid kumtaka Gareth Bale, 25 na beki
Rafael Varane, 22 limekataliwa na klabu hiyo ya La Liga (Daily Express),
Real Madrid wana uhakika wa kumsajili kwa pauni m… Read More
Uzinduzi wa jezi mpya Tifa Stars kuambata na tuzo maalumu.
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), kesho Jumatano linatarajia kuzindua
jezi mpya za timu za Taifa Tanzania, zitakazokuwa zikitumika katika
michuano mbalimbali, uzinduzi huo utakafanyika katika hoteli ya JB
Belmonte (PS… Read More
0 comments:
Post a Comment