Facebook

Thursday, 3 July 2014

Basi la mahabusu lashambuliwa na majambazi Dar

Baadhi ya mashuhuda wakwa wanashangaa na kutoamini tukio hilo linalosemekana lilikuwa kama muvi.
Baadhi ya mashuhuda wakiwa wanashangaa na kutoamini kutokea kwa tukio hilo linalosemekana lilikuwa kama muvi.
Basi la magereza lililokuwa limebeba mahabusu na wafungwa likisindikizwa na askari polisi limeshambuliwa kwa risasi na watu wenye silaha wanaosadikika kuwa ni majambazi, ameeleza shuhuda mmoja.
Watu hao wenye silaha walikuwa wakitokea kwenye kituo cha Nyerere jijini Dar es Salaam walilishambulia basi hilo na kuwajeruhi baadh ya askari.
Mahabusu waliokuwa kwenye basi hilo walianza kushangilia wakati tukio hilo likifanyika, huku ikisemekana kuwa lengo la shambulio hilo ni kuwatorosha mahabusu hao.
Gari la askari likiwa linasindikiza basi hilo la mahabusu, mbale yake ni gari ya wagonjwaa (ambulance).
Gari la askari likiwa linasindikiza basi hilo la mahabusu, mbale yake ni gari ya wagonjwaa (ambulance).
Taarifa zinasema kwamba baada ya kushambulia basi hilo, majambazi hao waliweza kukimbia mahali pasipojulikana.
Mpaka sasa hakuna taarifa yoyote kutoka jeshi la polisi na jeshi la magereza kuhusiana na tukio hilo la leo.
Upande wa basi hilo la mahabusu likionekana kupasuliwa kioo na watu hao wanaosadikika kuwa ni majambazi.
Upande wa basi hilo la mahabusu likionekana kupasuliwa kioo na watu hao wanaosadikika kuwa ni majambazi.

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment