Facebook

Wednesday, 9 July 2014

Filamu ya Biafra kuanza kuonyeshwa Nigeria hivi karibuni.

Photo: FILAMU YA BIAFRA KUANZA KUONESHWA NIGERIA
Filamu yenye utata kuhusu vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Nigeria katika miaka ya 1960, itaanza kuoneshwa katika majumba ya sinema kuanzia mwezi Agosti, baada ya wadhibiti filamu kuruhusu ioneshwe. Filamu hiyo- Half of a Yellow Sun, inayohusu vita vya Biafra ilikuwa ianze kuoneshwa mwezi Aprili, lakini bodi ya filamu nchini humo ilisema baadhi ya vipande katika filamu hiyo vilikuwa havikubaliki. Filamu hiyo imetengenezwa kutokana na kitabu kilichoandikwa na mwandishi maarufu wa vitabu Chimamanda Ngozi Adichie. Zaidi ya watu milioni moja walikufa katika vita hivyo, vilivyosababishwa na jaribio la kujitenga la majimbo ya kusini mashariki ya Nigeria. Kulikuwa na wasiwasi kuwa filamu hiyo huenda ingeleta mvutano wa kikabila.
 
Filamu yenye utata kuhusu vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Nigeria katika miaka ya 1960, itaanza kuoneshwa katika majumba ya sinema kuanzia mwezi Agosti, baada ya wadhibiti filamu kuruhusu ioneshwe. 
 Filamu hiyo- Half of a Yellow Sun, inayohusu vita vya Biafra ilikuwa ianze kuoneshwa mwezi Aprili, lakini bodi ya filamu nchini humo ilisema baadhi ya vipande katika filamu hiyo vilikuwa havikubaliki.
  Filamu hiyo imetengenezwa kutokana na kitabu kilichoandikwa na mwandishi maarufu wa vitabu Chimamanda Ngozi Adichie. Zaidi ya watu milioni moja walikufa katika vita hivyo, vilivyosababishwa na jaribio la kujitenga la majimbo ya kusini mashariki ya Nigeria. Kulikuwa na wasiwasi kuwa filamu hiyo huenda ingeleta mvutano wa kikabila.

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment