
Kocha wa Ujerumani Joachim Low amekimwagia sifa kikosi chake mara
baada ya kuifungisha virago timu ya Ufaransa katika mchezo wa robo
fainaili kwa ushindi wa goli 1-0.
Low amesema kuwa mbinu za kiuchezaji walizonazo wachezaji wake
zinaweza kuwafikisha katika hatua ya fainali katika michuano hii ya
Kombe la Dunia, hata hivyo aliendelea kusisitiza kuwa bado timu za taifa
za Marekani ya Kusini zina nafasi kubwa ya kulichukua Kombe hilo la
Dunia.
Kocha huyu pia aliwamwagia sifa walinzi wa timu zote mbili kwani
kulikuwa hakuna nafasi nyingi za kufunga zilizotengenezwa, pia
aliwasifia walinzi wake kwakufanikiwa kumbana mbavu Karim Benzema
asipate mwanya wa kuwaumiza.
Alisema kuwa kabla ya mchezo nilipitia kikosi cha Ufaransa nikagundua
wana wachezaji wazuri katika nafasi ya kiungo mkabaji, ambako Cabaye na
Pogba wamekuwa katika kiwango bora katika michuano hii wakicheza kwenye
nafasi hiyo ndio maana ni kafanya maamuzi ya kumtoa Philip Lahm
katikati na kumchezesha akitokea pembeni, huku Jerome Boateng akirudi
katika nafasi ya beki wa katikati nafasi iyokuwa imeachwa wazi na beki
Per Mertesacker.
Hatahivyo maamuzi hayo yaliweza kuzaa matunda.
Japokuwa beki Matt Hummels alitangazwa kama mchezaji bora wa mechi
lakini naamini hata mlinda mlango wetu Manuel Neuer ni mmoja kati ya
wachezaji bora duniani kwani aliweza kuokoa michomo mingi ya wazi katika
dakika za majeruhi za mchezo, alisikika kocha huyo wa Ujerumani
akisema.
Ujerumani itakutana na Brazil katika hatua ya nusu fainali mara baada ya kuifunga Colombia kwa bao 2-1.
Related Posts:
Barcelona yaanza ligi kwa ushindi mnono..
Barca imefungua msimu kwa ushindi mkubwa dhidi ya Elche
Lionel Messi alifunga mabao
mawili na kuisaidia Barcelona kuilaza Elche mabao 3-0 katika me… Read More
Kikosi cha taifa stars kitakachopambana na Morocco chatajwa.
Morocco ( Atlas Lions) v Tanzania ( Taifa Stars),
5 Septemba... Haya ni majina ya wachezaji wa
STARS yaliyotangazwa na mkufunzi mkuu, Martin
Nooij....
MAKIPA,
Deogratius Munish ( Yanga SC),
Mwadini Ally Mwadini ( Azam FC),… Read More
Manchester City yaigaraza Liverpool.
MABINGWA wa England, Manchester City, Jana Usiku wakiwa kwenye uwanja wao Etihad
wameonyesha kuwa hawana mzaha walipoitandika Timu iliyomaliza Nafasi ya
Pili Msimu uliopita, Liverpool,magoli 3-1 katika Mechi ya Ligi Kuu
… Read More
Hatimaye Lampard astaafu soka la kimataifa rasmi.
Frank lampard ametangaza kustaafu soka la kimataifa ikiwa tayali ameichezea timu hyo ya taifa mechi 106 na kuifungia mabao 26.
Lampard aliyeanza kucheza soka la kulipwa katika club ya WestHam na badae kwenda Chelsea am… Read More
KAULI YA BALOTELI BAADA YA KUTUA RASMI LIVERPOOL
"Nadhani nilifanya makosa kuondoka England,nilipenda kwenda Italy lakini nmegundua lile lilikua kosa"
>Akizungumzia huamisho wa Baloteli kocha wa Liverpool Brandan Rosgers amesema "Uhamisho huu umefata misingi ya kl… Read More
0 comments:
Post a Comment