KIUNGO mahiri wa kimataifa wa Hispania, Xavi anatarajia kutangaza
uamuzi wake wa kuondoka Barcelona Alhamisi hii wakati akijiandaa
kuhamia katika klabu ya Al Sadd ya Qatar.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 35 amekuwa akiitumikia
Barcelona kipindi chote na kuisaidia kushinda mataji 23 lakini
anataka kuamua kuondoka baada ya muda mwingi msimu huu
akiutumia akiwa benchi.
Xavi ambaye alikaribia kwenda Al Sadd kiangazi mwaka jana kabla
ya kushawishiwa kubakia Barcelona na meneja Luis Enrique,
anatarajiwa kukutana na wanahabari wiki hii kufafanua uamuzi wake
huku akitarajiwa kuaga Camp Nou katika mchezo wa La Liga dhidi ya
Deportivo La Coruna.
Rais wa Barcelona, Josep Maria Bartomeu amemuelezea Xavi kama
kiungo bora kabisa kuwahi kutokea katika historia ya klabu hiyo.
Xavi anaweza kuongeza medali zingine mbili kati ya nyingi alizonazo
kabla ya kuondoka, wakati Barcelona itakapokwaana na Athletic
Bilbao katika mchezo wa Kombe la Mfalme baadae mwezi huu kabla
ya kukabiliana na Juventus katika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya
Juni 6.
Tuesday, 19 May 2015
Xavi kuwaaga mashabiki wa Barcelona Alhamisi.
Related Posts:
Demba Ba atua rasmi Uturuki kwa £8m Demba Ba sasa kuvaa jesi ya Besiktas ya Uturuki Usajili mpya na mikataba mipya kwa wachezaji vinara ndio shughuli kuu inayoendelea sasa kabla msimu mpya wa michuano kuanza.. Pamoja na kasheshe zinazomuandama, Suarez s… Read More
Tetesi za usajili katika magazeti mbalimbali barani Ulaya. Kiungo wa Manchester City Yaya Toure, 31, amekataa kujiunga na Manchester United (Daily Star), kiungo wa Everton Ross Barkley, 20, anatazamwa na Man City kuziba nafasi ya Yaya Toure, iwapo atalazimisha u… Read More
Ferdinand asajiliwa rasmi QPR Beki wa zamani wa Manchester United Rio Ferdinand, 35, amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuichezea QPR. … Read More
Arsenal yamnasa Debuchy,Newcastle yakamilisha usajili wa Janmaat Arsenal imemsaini Fulbeki Mathieu Debuchy kutoka Newcastle. Debuchy, Miaka 28, alikuwa mmoja wa Wachezaji wa France waliocheza Kombe la Dunia huko Brazil na ameletwa Emirates kuchukua nafasi ya Bacary Sagna ambae … Read More
Toni Kroos atua rasmi Madrid. Kiungo wa Bayern Munich Toni Kroos amejiunga rasmi na Real Madrid kwa mkataba wa miaka sita kwa kitita ambacho hakikutajwa. Kroos, 24, alikuwa mchezaji muhimu katika kikosi cha Ujerumani kilichoishinda Argentina… Read More
0 comments:
Post a Comment