KIUNGO mahiri wa kimataifa wa Hispania, Xavi anatarajia kutangaza
uamuzi wake wa kuondoka Barcelona Alhamisi hii wakati akijiandaa
kuhamia katika klabu ya Al Sadd ya Qatar.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 35 amekuwa akiitumikia
Barcelona kipindi chote na kuisaidia kushinda mataji 23 lakini
anataka kuamua kuondoka baada ya muda mwingi msimu huu
akiutumia akiwa benchi.
Xavi ambaye alikaribia kwenda Al Sadd kiangazi mwaka jana kabla
ya kushawishiwa kubakia Barcelona na meneja Luis Enrique,
anatarajiwa kukutana na wanahabari wiki hii kufafanua uamuzi wake
huku akitarajiwa kuaga Camp Nou katika mchezo wa La Liga dhidi ya
Deportivo La Coruna.
Rais wa Barcelona, Josep Maria Bartomeu amemuelezea Xavi kama
kiungo bora kabisa kuwahi kutokea katika historia ya klabu hiyo.
Xavi anaweza kuongeza medali zingine mbili kati ya nyingi alizonazo
kabla ya kuondoka, wakati Barcelona itakapokwaana na Athletic
Bilbao katika mchezo wa Kombe la Mfalme baadae mwezi huu kabla
ya kukabiliana na Juventus katika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya
Juni 6.
Tuesday, 19 May 2015
Xavi kuwaaga mashabiki wa Barcelona Alhamisi.
Related Posts:
Di Maria awekwa kwando katika mechi ya Leo;Njia nyeupe Kuondoka Madrid.Imeripotiwa kwamba Angel Di Maria ameachwa kwenye kikosi cha Real Madrid kitachopambana na Atletico Madrid usiku wa leo baada ya jana kuthibitika kwamba ameomba kuuzwa. … Read More
Tetesi za usajili katika magazeti mbalimbali barani Ulaya na BantuTz SPORTS >Juventus na Roma wanataka kumsajili beki wa kati wa Manchester City Matija Nastasic, 21, huku Newcastle na West Ham wakimtaka beki wa kulia wa Man City Micah Richards, 26, (Manchester Evening News), >Manchester Unite… Read More
Di Maria aomba kuondoka Madrid;Khedira agoma kusaini mkataba mpya.Winga wa Argentina Angel Di Maria ameiambia Real Madrid kwamba anataka kuondoka Klabuni hapo. Di Maria amekuwa akihusishwa na Uhamisho wa kwenda Manchester United huku ikiripotiwa kuwa Meneja Louis van Gaal ana nia kubwa kuml… Read More
Mario Balloteli mbioni kutua Liverpool;Ada ya uhamisho yakubaliwa.Liverpool na AC Milan zimekubaliana Ada ya Uhamisho ya Pauni Milioni 16 ili Mario Balotelli ahamie Anfield. Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers alikuwa akihaha kutaka kuziba pengo la Straika wake Luis Suarez ambae amehamia Ba… Read More
Mario Balloteli mbioni kutua Liverpool;Ada ya uhamisho yakubaliwa.Liverpool na AC Milan zimekubaliana Ada ya Uhamisho ya Pauni Milioni 16 ili Mario Balotelli ahamie Anfield. Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers alikuwa akihaha kutaka kuziba pengo la Straika wake Luis Suarez ambae amehamia Ba… Read More
0 comments:
Post a Comment