Facebook

Sunday, 13 July 2014

Tetesi za usajili katika magazeti mbalimbali barani Ulaya.


 Salim Kikeke's photo.
Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers ataruhusiwa kutumia fedha zote, pauni milioni 75 za mauzo ya Luis Suarez kuimarisha kikosi chake (The Times), 
 
Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger anayetafuta kiungo mkabaji anapanga kuwachukua Sami Khedira, 27, na Lars Bender, 25 (Daily Telegraph), 
 
Hata hivyo Chelsea wapo tayari "kuuteka" mchakato wa Sami Khedira na kumsajili mchezaji huyo wa Real Madrid (Daily Mirror), 
 
Crystal Palace wanakaribia kumsajili Fraizer Campbell kutoka Cardiff City (Guardian), 
 
Newcastle wanakaribia kumsajili Emmanuel Riviere, 24, kutoka Monaco, mchezaji huyo amehusishwa pia na kwenda Arsenal, Stoke City na West Brom (Evening Chronicle)
 
 Arsenal na Tottenham wanamwania Loic Remy, 27, ingawa Newcastle huenda wakafanikiwa kumsajili mchezaji huyo wa QPR aliyecheza msimu uliopita kwa mkopo (Talksport),
 
 Stoke wako karibu kumsajili Bojan Krkic, 23, kutoka Barcelona (Daily Star), 
 
Inter Milan wanafikiria kumsajili beki kutoka Chile Gary Medel, 26 anayechezea Cardiff (Sky Sports),
 
 Manchester United na Chelsea wanamgombea kiungo Alex Song, 26, na Barcelona wako tayari kupokea pauni milioni 20 (Daily Star),
 
 Newcastle wamekubaliana na Montpellier kumsajili kiungo mshambuliaji Remy Cabella, 24 (Daily Express),
 
 West Ham wamepata upinzani kutoka Sevilla na AC Milan kumsajili mshambuliaji wa Ecuador Enner Valencia anayechezea Pachuca ya Mexico (Times), 
 
Chelsea wanafikiria kutoa dau la pauni milioni 7 kumchukua kiungo Adrien Rabiot, 19, kutoka Paris St-Germain (Daily Express), 
 
Real Madrid wanafikiria kumchukua mshambuliaji wa Manchester United Danny Welbeck kuziba nafasi ya Alvaro Morata anayetarajia kujiunga na Juventus (Daily Star), 
 Salim Kikeke's photo.
Arsenal tayari wametangaza dau la euro milioni 25 kwa Sami Khedira, ingawa Chelsea nao wanamtaka kiungo huyo wa Real Madrid (Daily Express), 
 
 Bebe, 23, anataka kuhamia Benfica kwa uhamisho wa kudumu. Bebe alikuwa kwa mkopo Pacos Ferreira ya Ureno (A Bola), 
 
Arsenal wanakaribia kumsajili beki wa kulia Javi Manquillo kwa mkopo kutoka Atlètico Madrid (Daily Telegraph),
 
 Tottenham wanajiandaa kutoa dau la pauni milioni 18 kumsajili mshambuliaji wa Swansea Wilfried Bony (Daily Star). 
 
Share tetesi hizi na wapenda soka wote. Tetesi nyingine kwenye magazeti na mitandao ya Jumapili tukijaaliwa. Cheers!

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment