
Ulaji wa supu ya pweza, karanga mbichi, muhogo mbichi, mbata kwa dai kwamba vinaongeza urijali (nguvu) kwa wanaume, kumeelezwa kuwa ni dhana potofu inayostahili kupigwa vita, kwa kuwa hakuna uhusiano kati ya urijali wa mwanamume na vitu hivyo wanavyokula.
Kauli hiyo imetolewa na Dk Cuthbert Maendaenda, ambaye alisema ipo haja ya wanaume kuangalia sababu za kudorora kwa uwezo wao na kufanya marekebisho, badala ya kudhani kwamba kuna dawa kutoka katika vyakula hivyo.
Katika miji mingi nchini kwa sasa, nyakati za jioni supu ya pweza na
karanga mbichi huuzwa, ambapo wauzaji wamekuwa wakinadi kama msaada wa
kurejesha heshima katika ndoa.
Unakubaliana na Dokta huyu kuwa ni dhana potofu tu au unampinga? Acha comment hapa chini.
Unakubaliana na Dokta huyu kuwa ni dhana potofu tu au unampinga? Acha comment hapa chini.
0 comments:
Post a Comment