Rais wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete
alifanyiwa upasuaji wa tezi dume
(prostrate) katika Hospitali ya Johns
Hopkins iliyoko Baltimore, Jimbo la
Maryland nchini Marekani.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kurugenzi
ya Mawasiliano ya Ikulu ya Tanzania, Rais
Kikwete amefanyiwa upasuaji huo baada ya
madaktari waliomfanyia uchunguzi wa afya
yake kujiridhisha kuwa Rais alikuwa anahitaji
matibabu ya aina hiyo.
Upasuaji huo ulikuchukua kiasi cha saa moja
unusu ambapo inaelezwa kuwa umefanyika
salama na kwa mafanikio makubwa.
Taarifa hiyo inasema hali ya Rais Kikwete
inaendelea vizuri japo bado yuko wodini
akiendelea kuwa chini ya uangalizi wa
madaktari na kupatiwa tiba.
Sunday, 9 November 2014
Kikwete afanyiwa upasuaji wa tezi dume
Related Posts:
Mitambo ya kuzalisha Umeme wa gesi yawashwa rasmi Tanzania.Mkurugenzi mtendaji wa shirika la umeme nchini injinia Felchesmi Mramba amesema jana wamewasha rasmi mitambo ya kuzalisha umeme wa gesi iliyopo Ubungo jijini Dar es Salaam. … Read More
Lowassa aahidi kuweka kipaumbele katika utoaji wa Elimu ya Kilimo.Mgombea urais wa vyama vinavyounda UKAWA Mh Edwad Lowassa amesema akichaguliwa kuwa Rais atahakikisha kuwa kipaumbele cha elimu pia kinatolewa kwa wakulima wafugaji na makundi mengine hatua itakayowawezesha kutekeleza majukum… Read More
Dr.Magufuli aahidi kufungua milango ya kiuchumi na kudumisha Aman alipokuwa Kigoma.Chama cha Mapinduzi kupitia mgombea wake John Magufuli katika Serikali ya awamu ya tano iwapo itapewa ridhaa yaa waTanzania imeahidi kuendelea kufungua milango ya kiuchumi kwa mikoa inayopakana na nchi jirani Kigoma ikiwemo h… Read More
Lowassa aitikisa Bariadi. Siku ya leo Mgombea Urais kupitia tiketi ya CHADEMA, Mh.Edward Ngoyai Lowassa alikuwa katika mji wa Bariadi na kujaza Umati mkubwa. Mh.Lowassa amejimadi kuimarisha huduma za jamii kama elimu, afya, maji na makazi. … Read More
Ratiba ya kampeni siku ya leo kwa wanaogombea kiti cha Urais :Dr.Magufuli na Mh.Lowassa.BantuZ:-UCHAGUZI MKUU TANZANIA 2015 ★Lowassa siku ya leo atakuwa akifanya kampeni mkoa wa Kagera maeneo mawili ambayo ni Karagwe na Kyerwa.Kesho Muleba na Bukoba mjini na Jumapili atakuwa Ngara mkoa wa Kagera. ★As… Read More
0 comments:
Post a Comment