Facebook

  • Tutorial 1

    This is Trial

  • Tutorial 2

    This is slide 2 description. Go to Edit HTML and replace these sentences with your own words. This is a Blogger template by Lasantha - PremiumBloggerTemplates.com...

  • Tutorial 3

    This is slide 3 description. Go to Edit HTML and replace these sentences with your own words. This is a Blogger template by Lasantha - PremiumBloggerTemplates.com...

Saturday 12 March 2016

UVUMILIVU UMEMSHINDA MANARA, AJA NA TAKWIMU NANI ANASTAHILI KUITWA WA KIMATAIFA.

Haji Manara-Afisa habari Simba SC
Waungwana kila uchwao kwenye jiji hili na viunga vyake sambamba na maeneo mengi ya nchi, kuna neno wa ‘kimataifa’ hulisikia likiimbwa.
Waimbaji wakuu wa neno hilo ni mashabiki wa Yanga wakiongozwa na mpiga zumari wao aliyeacha kazi yake na kujigeuza muimbaji.
Kinyume chake hilo neno klabu ya Simba huitwa wa ‘mchangani’ au wa ‘matopeni’. Wengi wananilaumu kuwa kwa nini huwa sijibu neno lolote la ajabu kwa Yanga. Jibu langu ni jepesi tu, lazima tujitofautishe msemaji wa klabu na mropokaji wa klabu.
Mimi hupenda kuzungumzia issues sio porojo au lugha za uchochoroni. Haiwezekani nikawa kiongozi kisha nikaongea lugha za mashabiki ‘maandazi’.
Kwa hiyo mtaniwia radhi wapenzi wa mpira kwa kutokuwa muimbaji wa ngonjera za uchochoroni. Mara zote nitabaki msemaji wa klabu kubwa nchini na ntaongea facts kwa kadri zilivyo.
Wadau zisomeni sifa za kimataifa kwa klabu ya Simba nje ya nchi halafu zifananisheni na timu nyingine nchini.
Walau kama zitafikia nusu tunawaruhusu watafute tusi jipya. Ombi langu kwenu isambazeni taarifa hii katak kila mtandao wa kijamii kisha waseme wao wanaojiita wa kimataifa.
Simba ndiyo timu ya kwanza nchini kupanda ndege na hii ilikuwa mwaka 1963 tena wakati huo taifa la Tanzania halikuwa limeundwa, ilikwenda Ethiopia kwa mwaliko wa rais wa taifa hilo Haile Selassie
Simba ndiyo timu ya kwanza kuvaa jezi na hii ilikuwa 1938 ilipocheza na kombaini ya mabaharia wa meli zilizotia nanga kwenye bandari ya Dar es salaam.
Simba ndiyo timu ya kwanza kuvaa viatu nchini na hii ilikuwa1949 ilipocheza na kombaini ya jeshi la majini Navy ya Afrika Kusini.
Simba ndiyo timu ya kwanza kuwa na basi lake yenyewe na hili lilinuliwa mwaka1968.
Simba ndiyo timu ya kwanza kumiliki jengo lake lenyewe na hili lilizinduliwa 1971.
Simba ndiyo timu ya kwanza kuwa bingwa wa ligi kuu nchini1966.
Simba ndiyo timu ya kwanza kuwakilisha nchi na hii ilikuwa 1967.
Simba klabu ya kwanza nchini kwenda Ulaya na hii ilikuwa 1974 ilipokwenda Poland
Simba ndiyo timu ya kwanza kuwa mabingwa wa Afrika Mashariki na kati na hii ilikuwa 1974.
Simba ndio mabingwa wa kihistoria wa Afrika Mashariki na Kati, ndiyo timu iliyochukua ubingwa mara nyingi kuliko klabu yeyote Afrika Mashariki na Kati (Champs off all time.)
Simba ndiyo timu pekee nchini iliyowahi kufika nusu fainali ya klabu bingwa Afrika na hii ilikuwa1974.
Simba ndiyo timu pekee nchini na Afrika Mashariki kufika fainali ya kombe la Caf na hii ilikuwa1993.
Simba ndio timu inayoshikilia rekodi Afrika kama si duniani kwa kufungwa na Mufurila Wonderers ya Zambia magoli 4-0 na kwenda kuibamiza 5-0 kwao, mbele ya rais wao Kenneth Kaunda. Hii haijafanywa na klabu yeyote Afrika na nina mashaka duniani, hii ilikuwa 1979.
Simba ilicheza katik hatua ya makundi ya klabu bingwa Afrika 2003 kwa mafanikio makubwa kulinganisha na timu yoyote nchini.
Simba ndiyo timu pekee kuivua ubingwa klabu bingwa Afrika nadi Zamalek hii ilikuwa pia 2003.
Simba ndiyo klabu pekee nchini kuzifunga timu zote za mataifa ya kiarabu kuanzia
Waliowatoa mwaka jana Etoile du Sahel (Tunisia)
Widad Casablanca (Morocco)
El Setif (Algeria)
El Harach (Algeria)
halaf tumezifunga timu zote kubwa za Misri Zamelek,Al Ahly, Arab Contractors, Ismailia, Mehala, Al kubra na timu nyingine mnajua huwa inafanywaje ikigusa kule.
Pia imeshaitoa El Merekh ya Sudan 1994 katak klabu bingwa ya Afrika. Simba pia imeshazifunga miamba ya Afrika Magharibi kuanzia Asec, Asante Kotoko, Hafia ya Guinea hata mabingwa wa kihistoria wa Zambia Nkana Red Devils.
Tukirudi juu Simba ndiyo timu ya kwanza kuvaa suti na hii ilikuwa 1974 ilipokwenda Poland.
Simba ndiyo klabu pekee nchini kujenga jengo lake yenyewe kwa nguvu za wanachama na mashabiki, wenzetu ni mkopo na msaada toka kwa mzee Karume100%, Simba ilipewa kiasi flan na mzee karume baada ya jengo kukamilika na hii ilikuwa mwanzoni mwa miaka ya 70.
Angalia idadi ya wachezaji wa Simba walioenda Ulaya kucheza soka la kulipwa.
Nico Njohole
Deo Njohole
Kassim Matitu
George Kulagwa
Huku ikiwa na makumi ya nyota wake kadhaa waliowahI kutapakaa sehemu mbalimbali duniani.
Nikutajie wachache.
Khalid Abeid
Haidar Abeid
Martin Kikwa
Athman Mambosasa
Zamoyoni Mogella
Hamis Gaga
Lilla Shomari
Iddi Pazi
Kiwelu Mussa
George Masatu
Hussein masha na wengine wengi.bila kumsahau nguli wa sasa mbwana samata.mutoto ya msimbazi.
Na hapa kumbukumbu zikae vizuri wazee wangu mimi, Sunday na Kassim Manara wakati wanaenda kucheza Ulaya hawakuwa wachezaji wa Yanga, walikuwa wakicheza Pan African.
Nimalizie kwa kuwaambia FIFA ilizitaja timu bora za karne kwa kila nchi kwa Tanzania Simba ilitajwa ndio timu bora ya karne na wenye mpira wao FIFA. Nenda kwenye rekodi za Caf ndio utajua nani wa kimataifa baina ya cc na wao.
Porojo za mjini ntakuwa nimezimaliza sasa na anayebisha abishe kwa data. Wakoloni wetu walitufundisha hivi…No reaserch no data no right to speak.Tafsiri isiyo rasmi, hujafanya utafiti na huna takwimu funga bakuli lako.
Asanteni na nendeni mkawaambie.
Haji S Manara
Msemaji wa klabu bora ya muda wote Tanzania (best club of all time)
Ukiona errors zipotezee jadili issues na nnaruhusu challenges kama zipo
Porojo peleka kuleeeeeee..
Nini maoni yako

Friday 11 March 2016

Hawa ndio Mawaziri wa Rais Dkt Magufuli waliopewa kibali cha kusafiri Nje ya Nchi.

Rais John Magufuli ametoa kibali kwa Mawaziri wawili kusafiri nje ya nchi, wameruhusiwa kwenda nchini Vietnam kujifunza mbinu za kuinua kilimo na kujenga viwanda

-Mawaziri wawili waliopata kibali hicho ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage na Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba.

Saturday 6 February 2016

Ratiba ya Soka katika ligi mbalimbali barani Ulaya Leo Jumamosi.

RATIBA YA SOKA LEO JUMAMOSI 06/02/2016
★Barclays Premier League
3:45 PM - Manchester City vs Leicester City
6:00 PM - Aston Villa vs Norwich City
6:00 PM - Liverpool vs Sunderland
6:00 PM - Newcastle United vs West Bromwich Albion
6:00 PM - Stoke City vs Everton
6:00 PM - Swansea City vs Crystal Palace
6:00 PM - Tottenham Hotspur vs Watford
8:30 PM - Southampton vs West Ham United

★Spanish Primera División
6:00 PM - Atletico Madrid vs Eibar
8:15 PM - Rayo Vallecano vs Las Palmas
10:30 PM - Athletic Bilbao vs Villarreal
07/02/2016
12:05 AM - Sporting Gijon vs Deportivo La Coruña

★German Bundesliga
5:30 PM - Eintracht Frankfurt vs VfB Stuttgart
5:30 PM - FC Ingolstadt 04 vs FC Augsburg
5:30 PM - Hannover 96 vs Mainz
5:30 PM - Hertha Berlin vs Borussia Dortmund
5:30 PM - Schalke 04 vs VfL Wolfsburg
8:30 PM - Bayer Leverkusen vs Bayern Munich

★Italian Serie A
8:00 PM - Bologna vs Fiorentina
10:45 PM - Genoa vs Lazio

★French Ligue 1
4:00 PM - AS Monaco vs Nice
7:00 PM - Angers vs Lyon
10:00 PM - Bastia vs Troyes
10:00 PM - Caen vs Stade de Reims
10:00 PM - GFC Ajaccio vs Guingamp
10:00 PM - Lorient vs Montpellier
10:00 PM - Toulouse vs Nantes

~Abel Alvaro

Rosicky Nje miezi mitatu.

Kiungo wa kati wa kilabu ya Arsenal Tomas Rosicky hatochezea timu yake kwa kipindi cha miezi mitatu kutokana na jeraha.Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 35 ambaye kandarasi yake inakamilika katika msimu wa joto,alipata jeraha jingine la paja wakati wa mechi dhidi ya Burnley siku ya jumamosi baada ya kipindi cha miezi saba akiuguza jereha.Mchezaji huyo wa taifa la Czech alijiunga na Arsenal mnamo mwezi Mei mwaka 2006.

Alipoulizwa iwapo Rosicky ameichezea Arsenal mechi yake ya mwisho,Wenger alijibu:Natumai hapana ,lakini jeraha hilo ni baya sana.Rosicky ambaye aliichezea Arsenal mara 246 alisaini mkataba wa mwaka mmoja msimu uliopita.

Wakati huohuo,Wenger amethibitisha kwamba mshambuliaji Danny Welbeck atarudi kuwachezea wachezaji wa Arsenal wasiozidi umri wa miaka 21 siku ya ijumaa.Mchezaji huyo wa Uingereza,mwenye umri wa miaka 25,ameuguza jereha tangu mwezi Aprili 2015 baada ya kupata jeraha hilo katika mechi iliotoka sare ya 0-0 dhidi ya Chelsea.

Friday 5 February 2016

Hili ndilo Baraza la Mawaziri Vivuli lilikotajwa leo bungeni.

BARAZA KIVULI LA MAWAZIRI

1.Wizara ya Ofisi ya Rais, Tamisemi, Utumishi na
Utawala Bora.
Mawaziri – Jaffar Michael
Naibu Waziri – Joseph Nkundi na Ruth Mollel

2.Wizara ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano
na Mazingira
Waziri – Ali Saleh Abdalla
Naibu Waziri – Pauline Gekul

3.Ofisi ya Waziri Mkuu: Sera, Bunge, Kazi Vijana,
Ajira na Walemavu
Waziri – Esther Bulaya
Naibu – Yusuph Makame na Maftah Abdalla

4.Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
Waziri – Magdalena Sakaaya
Naibu Waziri – Emmaculate Swari

5.Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
Inj. James Mbatia
Naibu Waziri Willy Kombucha

6.Wizara ya Fedha na Mipango
Waziri – Halima Mdee
Naibu Waziri – David Silinde

7.Wizara ya Nishati na Madini
Waziri – John Mnyika
Naibu Waziri – John Heche

8.Wizara ya Katiba na Sheria
Waziri – Tundu Lissu
Naibu Waziri Abdalla Mtolela

9.Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afika
Mashariki, Kikanda na Kimataifa.
Waziri – Peter Msigwa
Naibu Waziri – Riziki Shaghal

10.Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
Waziri – Juma Omari
Naibu Waziri Mwita Waitara

11.Wizara ya Mambo ya Ndani
Waziri – Godbless Lema
Naibu Waziri Masoud Abdalla

12.Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya
Makazi.
Waziri – Wilfred Lwakatare
Naibu Waziri – Salum Mgoso

13.Wizara ya Maliasili na Utalii
Waziri Esther Matiko
Naibu Waziri– Cecilia Pareso

14.Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.
Waziri Anthony Komu
Naibu Waziri Cecil Mwambe

15.Wizara ya Elimu, Sayansi Teknolojia na Ufundi
Waziri – Suzan Lyimo
Naibu Waziri Dkt. Ali Suleiman Yusuph

16.Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto
Waziri – Dkt. Godwin Mollel
Naibu Waziri Zubeda Sakul

17.Wizara ya Habari, Utamadu, Wasanii na Michezo
Waziri – Joseph Mbilinyi
Naibu Waziri – Devotha Minja

18.Wizara ya Maji na Umwagiliaji
Waziri – Hamidu Hassan
Naibu Waziri– Peter Lijualikali.

Tuesday 2 February 2016

Kiungo wa Manchester United ajiunga na Hull City.

Kiungo wa Klabu ya Manchester United,Nick Powell amejiunga na klabu ya Hull City baada ya kukosa nafasi katika klabu hiyo na atakuwa Hull City kwa mkopo hadi mwisho wa msimu huu kumalizika.

Manchester United,Arsenal zatuma ofa kwa Mshambuliaji wa PSG.

Vilabu vya Arsenal na Manchester United vyote vinashiriki ligi kuu nchini Uingereza vimeripotiwa kuangalia uwezekano wa kumsajili Mshambuliaji hatari Edison Cavan ambaye hana furaha katika klabu ya PSG ya nchini Ufaransa.

Mshambuliaji huyo ambaye anapendelea zaidi kucheza nafasi ya ushambuliaji hana furaha katika klabu ya PSG kutokana na kuchezeshwa sehemu ambayo haifurahi,Cavani anapatikana kwa £55m endelea kutembelea www.bantuz.com na kwa taarifa za usajili kwa wakati na muda muafaka like na tembelea page yetu facebook :--> http://www.facebook.com/bantuzfanspage

Monday 1 February 2016

Beki wa Arsenal asajiliwa rasmi Bordeaux.

Klabu ya Arsenal imethibitisha mlinzi wake wa pembeni Mathieu Debuchy amejiunga na klabu ya Bordeaux kwa mkopo hadi mwisho wa msimu.

Huku taarifa za awali zinasema;Klabu ya Manchester United ilikuwa imetuma maombi kwa klabu ya Arsenal kuhitaji kuhitaji huduma ya mlinzi huyo lakini kocha wa Arsenal ameamua kukubali ofa ya klabu ya Bordeaux.

-www.bantuz.com