Facebook

Tuesday 22 September 2015

Ferguson afunguka kuhusiana na mambo yaliyokuwa nyuma ya pazia katika utawala wake Man United.


1.Fergie anakiri kuwa kabla hata Man City hawajamnyemelea Aguero,Atletico waliiambia Man United itoe £35m kumpata Aguero lakin Fergie aliona nyingi na baadae akaenda Man City kwa £38m coz walikuwa desperate.

2.Fergie anasema kwa mara ya kwanza waliambiwa na scouts kuna wonderkid aitwae Muller huko Ujerumani na ana miaka 10,walitaka kumsajili ila muller aliamua kubaki katika kituo cha kukulia vipaji cha Bayern Munich.

3.David Moyes alikuwa chaguo la 6 la Ferguson katika kuichukua Man United.Chaguo la kwanza lilikuwa ni Pep Guardiola baada ya kukutanaa naye Marekani wakati wa likizo.Mourinho alikuwa chaguo la pili ila alishamuahidi Abramovic kwamba angerejea,Klopp alikuwa chaguo la tatu ila alitaka kusaini mkataba mpya Dortmund.Ancelloti na Van Gaal walikuwa chaguo la nne na la tano lakini walikuwa na timu tayari huku Ancelloti akiwa mrithi wa Mourinho.Na hapo ndipo Fergie na bodi ya Man United wakaamua kumchukua Moyes.

4.Fergie anasema dunia kwa sasa ina "world class players" wawili tu nao ni Messi na Ronaldo.na anasema amewahi fundisha 'world class player' wanne tu nao ni Scholes,Giggs,Ronaldo na Cantona.

Sir Alex Ferguson
"kwa muda wangu wote wa miaka 26 klabuni Old Trafford nimesajili wachezaji wa kiwango cha juu, daraja la kwanza wanne tu ambao ni Eric Cantona, Ryan Giggs, Cristiano Ronaldo na Paul Scholes" 
5.Fergie anasema alipinga upandishwaji mkubwa wa mshahara wa Rooney 2010 ambapo Rooney alisaini miaka 5 na alikuwa akilipwa £180,000 ambapo ni mara mbili ya alichokuwa akilipwa Fergie.Ndipo Fergie akakutana na Joel Glazer na kumwambia haiwezekani na wakakubaliana hakuna mchezaji atakayelipwa zaidi Ya SAF na ndipo SAF alipoongezewa mshahara.
 Sir Alex Ferguson!"Sijakubali mchezaji yeyote klabuni kwangu anizidi mshahara"
 
6.Mnamo mwaka 2010 Fergie alitaka kumsajili Balotelli ila washauri Fergie ndani ya Italia walimshauri Fergie kuwa ni risky sana kumsajili Balotelli kutokana na matendo yake.

7.Fergie anasema Mino Raiola ndo alikuwa chanzo cha Pogba kuondoka man united coz walikuwa hawapatani na alijali pesa kuliko kipaji cha Pogba.

8.Fergie anasema kosa kubwa la Moyes ilikuwa kuwafukuza staff nzima aliyoiacha na anampongeza Van Gaal kwa kumuweka giggs pale kwasababu anaijua vzuri club

9.Fergie anakiri kuwa huwa anaangalia Press conference za Van Gaal kwasababu zinashangamsha na kufurahisha.

10.Fergie Anasema walikuwa karibu kumsajili Varane kabla Zidane hajaingilia kati na kumshauri aende Madrid.

11.Fergie anasema wachezaji wa united walikuwa wakimrushia matani Ronaldo kwasababu alikuwa hawezi kupita mbele ya kioo bila kujiangalia, alikuwa ni mtu wa kujiangalia sana.

12.Katika kipindi chake anasema watu wenye influence sana juu ya wachezaji wengine walikuwa ni Roy Keane,Bryan Robson na Steve Bruce.

0 comments:

Post a Comment