Thursday, 24 April 2014
Ivo.."Ntaliacha taulo linalowapa kiwewe wapinzani"..............fuatilia hapa................
INAWEZA kuwa habari njema kwa timu zitakazocheza na Simba msimu ujao wa Ligi Kuu Bara au mechi za kirafiki.
Kipa wa timu hiyo, Ivo Mapunda amesema ataacha kulitumia taulo lake katika michezo atakayocheza ili kuwatoa wasiwasi mashabiki wa timu pinzani.
Tangu alipokuwa akiichezea Gor Mahia ya Kenya msimu uliopita, Mapunda amekuwa akitumia taulo ambalo hulitundika katika nyavu za goli analodaka ili kujifuta jasho mikono yake pindi inapoonekana kuwa inateleza kuokoa mashuti ya timu pinzani.
Hata hivyo, mashabiki wengi wamekuwa wakilihusisha taulo hilo na imani za kishirikina.
Taulo la Mapunda liliibua tafrani Jumamosi iliyopita katika mchezo wa Simba na Yanga uliochezwa Uwanja wa Taifa, baada ya dakika 56 Yanga kukosa bao la wazi huku kipa huyo akiwa ametoka langoni ambapo kila walipopiga mpira ulikuwa ukiwagonga mabeki wa Simba.
Ndipo Didier Kavumbagu akalifuata taulo hilo na kwenda kulirusha kwa mashabiki wa timu yake japokuwa halikuweza kuwafikia.
Mapunda alisema: “Nimeamua kuachana na taulo langu ili kuwatoa wasiwasi wapinzani wangu, unajua wengi wanadhani lina mambo ya uchawi sasa ili wacheze wakiwa huru na kujituma sitaingia nalo uwanjani badala yake nitabuni kitu kingine ambacho kitakuwa maarufu kama taulo.
“Ninachofanya ni kuwapa burudani mashabiki wala hakuna kitu kingine cha ziada, lakini watu hawaelewi tazama Yanga walivyogombea taulo langu, mataulo yangu yote hayana uchawi wowote.”
Related Posts:
BantuTz LIVESTREAMING:-ANGALIA MECHI ZOTE ZA LEO UEFA CHAMPIONS LEAGUE KATIKA SIMU,TABLET AU COMPUTER YAKO.Angalia Mechi zote za UEFA CHAMPIONS LEAGUE 'LiveStreaming' kupitia Simu,Computer au Tablet yako. Utaangalia mechi hiyo bila kukwama au kukatika kwa matangazo ya mechi hiyo hata kidogo. Utafurahia kuangalia mechi hiyo kama ut… Read More
BantuTz MAGAZINE-Soma kilichoandikwa katika Magazeti ya leo Novemba 27. BantuTz MAGAZETI:Ni miongoni mwa huduma bora kabisa tunazozitoa ili wewe mdau wa Bantu usipitwe na habari,stori au taarifa yoyote ile.Tunakuletea kila tunachokipata kwa wakati na muda muafaka.Soma kilichoandikwa… Read More
Instagram yamuweka Balotelli matatani. Shirikisho la soka FA linachunguza ujumbe wa Instagram wa mshambuliaji wa Liverpool Mario Balotelli unaodaiwa kuwa ni wa kibaguzi. Ballotel mwenye umri wa miaka 24 akijibu shutma dhidi yake kutokana na ujumbe wake mtan… Read More
Wachezaji wa Real Madrid wakabidhiwa magari ya kifahari na kampuni ya Audi. Kampuni ya magari ya Audi imewakabidhi wanandinga wa klabu ya Real Madrid magari yao aina ya Audi huko Ciudad Real Madrid, ambapo wanandinga hao walikabidhiwa funguo zao kwenye sherehe maalum, ya kuadhimisha miaka kumi na mo… Read More
BantuTz MAGAZINE-Soma kilichoandikwa katika Magazeti ya leo Desemba 2 BantuTz MAGAZETI:Ni miongoni mwa huduma bora kabisa tunazozitoa ili wewe mdau wa Bantu usipitwe na habari,stori au taarifa yoyote ile.Tunakuletea kila tunachokipata kwa wakati na muda muafaka.Soma kilichoandikw… Read More
0 comments:
Post a Comment