Facebook

Saturday 30 January 2016

Chelsea yakamilisha usajili wa beki 'kisiki' kutoka Marekani.

Klabu ya Chelsea imethibitisha kunasa saini ya beki wa kati Matt Miazga kutoka klabu ya New York Red Bulls inayoshiriki Ligi Kuu Nchini Marekani. Matt Miazga amesaini mkataba wa miaka minne na nusu huku ada ya uhamisho ikiwa haijawekwa wazi.

Huu ni usajili wa pili katika Klabu ya Chelsea mara baada ya hapo jana kufanikiwa kukamilisha usajili wa mshambuliaji Alexandre Pato.

Endelea kutembelea www.bantuz.com kwa taarifa mbalimbali za usajili barani Ulaya.

0 comments:

Post a Comment