Facebook

Saturday 23 January 2016

Chicharito Mchezaji Bora Amerika ya Kaskazini.

Hernandez ‘Chicharito’ ametwaa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka 2015 kwa Kanda ya Kisoka ya CONCACAF inayojumuisha Nchi za Marekani ya Kati na Kaskazini pamoja na Visiwa vya Carribean.

Tuzo hiyo imetokana na Kura za Makocha na Manahodha wa Timu za Taifa pamoja na Wanahabari maalum na Mashabiki.

Baada ya kuihama Manchester United na kuhamia Klabu ya Bundesliga ya huko Germany, Bayer Leverkusen, Chicharito amewika mno na pia kuisaidia Nchi yake Mexico kuifunga USA 3-2, huku yeye akifunga 1, wakati wanafuzu kuiwakilisha CONACAF kwenye Fainali za Mashindano ya FIFA ya Kombe la Mabara za 2017 zitakazochezwa huko Urusi.

Akitwaa Tuzo hii, Chicharito aliwabwaga Bryan Ruiz wa Costa Rica na Andres Guardado wa Mexico.

0 comments:

Post a Comment