Facebook

Saturday, 23 January 2016

Chicharito Mchezaji Bora Amerika ya Kaskazini.

Hernandez ‘Chicharito’ ametwaa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka 2015 kwa Kanda ya Kisoka ya CONCACAF inayojumuisha Nchi za Marekani ya Kati na Kaskazini pamoja na Visiwa vya Carribean.

Tuzo hiyo imetokana na Kura za Makocha na Manahodha wa Timu za Taifa pamoja na Wanahabari maalum na Mashabiki.

Baada ya kuihama Manchester United na kuhamia Klabu ya Bundesliga ya huko Germany, Bayer Leverkusen, Chicharito amewika mno na pia kuisaidia Nchi yake Mexico kuifunga USA 3-2, huku yeye akifunga 1, wakati wanafuzu kuiwakilisha CONACAF kwenye Fainali za Mashindano ya FIFA ya Kombe la Mabara za 2017 zitakazochezwa huko Urusi.

Akitwaa Tuzo hii, Chicharito aliwabwaga Bryan Ruiz wa Costa Rica na Andres Guardado wa Mexico.

Related Posts:

  • Hizi ni tetesi zote za Usajili wa wachezaji barani Ulaya siku ya leo.Manchester United wanakaribia kutoa dau la pauni milioni 25 kumtaka mshambuliaji wa Liverpool Raheem Sterling, 20 (Mirror), Chelsea wanataka kumsajili Radamel Falcao kwa mkopo kutoka Monaco. Falcao, 29, amefunga mabao manne k… Read More
  • McClaren kocha mpya Newcastle. Steve McClaren anatarajiwa kuthibitishwa kuwa Meneja mpya wa Klabu ya Ligi Kuu England Newcastle Wiki ijayo. McClaren, mwenye Miaka 54, ni Meneja wa zamani wa England na pia aliwahi kuwa Meneja Msaidizi chini ya… Read More
  • Man City yamuwekea dau Alex SongManchester City imeonyesha nia ya kupata huduma ya mchezaji wa Barca Alex Song ambaye msimu huu alikuwa akicheza kwa mkopo timu ya Westham inayoshiriki.Alex aliyerudi nyumbani Barcelona anaweza kuuuzwa jumla na kujiunga na … Read More
  • Benitez amtaka Laurent KoscielnyKocha mpya wa Real Madrid Benitez anataka kumsaini beki wa Arsenal Laurent Koscielny. Ni imani ya kocha wa zamani wa Liverpool na Chelsea atampata Mfaransa huyo kuwa msaidizi wa Sergio Ramos katika ulinzi. Koscielny alisai… Read More
  • Juventus yamnasa mshambuliaji hatari Paulo Dybala Mabingwa wa ligi kuu ya Italia Juventus leo hii wamethibitisha kukamilisha usajili wa mshambuliaji Paulo Dybala kutoka katika klabu ya Palermo kwa kitita cha euro milioni 32. Mshambuliaji huyo mwenye umri … Read More

0 comments:

Post a Comment