Facebook

Saturday 23 January 2016

TETESI ZA USAJILI BARANI ULAYA: NEYMAR, TEIXEIRA, MESSI, WENGER, ADEBAYOR, BERAHINO, KLOPP, THIAGO SILVA, PETR CECH

Manchester United na Manchester City watashindana kuipigania saini ya mshambuliaji wa Barcelona Neymar, 23 (Chanzo Gazzetta)

United wanakaribia pia kumpata kiungo wa Benifica Renato Sanches, 18, na wanategemewa kulipa paundi millioni 30. (Chanzo Daily Mail)

Mshambuliaji wa Manchester City Sergio Aguero ameongea na mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi, 28, kuhusu kumshawishi kuhamia Manchester City. (Chanzo Sky Sports)

Wakati huo huo, Meneja wa City Manuel Pellegrini hatagemei kununua au kuuza mchezaji yoyote mwezi huu Januari (Chanzo Manchester Evening News)

Bosi wa Arsenal mzee Arsene Wenger, 66, anajiandaa kuongeza mkataba mpya na klabu ya Arsenal. (Chanzo Sun)

Washika Bunduki wanafikiria pia kuongeza dau la pili kwa beki wa kushoto wa Leicester City Ben Chilwell, 19, baada ya ofa ya paundi millioni 3.5 waliyoitoa awali kukataliwa. (Telegraph)

Bosi wa Manchester United Louis van Gaal anapanga kumchukua beki wa kushoto wa Southampton Ryan Bertrand, 26, lakini itamlazimu kulipa zaidi ya paundi millioni 20. (Chanzo Daily Star)

United wanaweza wakamchukua beki wa zamani wa Chelsea na Arsenal Ashley Cole. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 35 yuko huru kwa sasa baada ya kuondoka klabu ya Roma ya nchini Italia.(Chanzo Independent)

Bosi wa Liverpool Jurgen Klopp amesema klabu yake haitoa pesa nyingi zaidi kwa mshambuliaji wa Shakhtar Donest Alex Teixeira, 26. (Chanzo Daily Telegraph)

Majagoo hao wa jiji bado wako kwenye mazungumzo na klabu ya nchini Ukrain Shakhtar juu ya makubaliano ya Teixeira, na wanafikiria kuongeza pesa kidogo kwenye ofa ya paundi millioni 24.6 waliyoitoa awali kwa mshambuliaji huyo wa Brazil. (Chanzo Guardian)

Chelsea wamewafata Paris St-German juu ya dili la kumsajili beki wa kati Thiago Silva, 31, mwishoni mwa msimu. (Chanzo Tuttomercatoweb – kwa Ligha ya Kiitalia)

Wakati huo huo, Chelsea wamemfanya kocha Massimiliano Allegri, 48, wa Juventus kuwa chagua la kwanza kama kocha atakayekuja kuingoza klabu hiyo msimu ujao. (Chanzo Sun)
Crystal Palace watalazimika kumlipa Adebayor paundi 77,000 kwa wiki endapo watataka kumsajili mshambuliaji huyo kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili. (Chanzo Mirror)

Winga wa Tottenham Andros Townsend, 24, na mshambuliji wa West Brom Saido Berahino, 22, wanatamani kuhamia Newcastle – Lakini juhudi za Newcastle United kuwasajili wachezaji hao zinazidi kugonga mwamba. (Chanzo Newcastle Chronicle)

Swansea City wanaonekana kumtaka mshambuliaji wa Barcelana Sandros Ramirez, lakini wanaweza wakapata upinzani kutoka kwa Tottenham. (Chanzo Daily Mail)

Golikipa Petr Cech, 33, asingetakiwa kuondoka Chelsea, amesema bosi wa The Blues Hiddink.(Chanzo Times) Hizi ni baadhi ya habari tulizozipata leo,

Tetesi nyingine tukutane kesho panapo majaaliwa.

0 comments:

Post a Comment