Facebook

Saturday 23 January 2016

Man United yakaribia kunasa saini ya kiungo chipukizi Renato Sanchez.

Klabu ya Manchester United inakaribia kunasa saini ya kiungo Chipukizi mwenye miaka 18,Mreno Renato Sanchez anayekipiga katika klabu ya Benfica.

Kiungo huyo ameshafunga magoli mawili katika mechi 13 tangia alipopandishwa kutoka timu ya vijana ya Benfica.

Viongozi wa Manchester United walikutana na wawakilishi wa Renato hapo jana (Ijumaa) katika jiji la London huku kiungo huyo akiwa na kizuizi katika mkataba wake cha Paundi ml 60 lakini viongozi wa Manchester United wanajaribu kuwashawishi Benfica kushusha dau hilo.

Kiungo huyo ameweza kuteka macho ya Wadau mbalimbali wa soka hususan ufundi alionao na nguvu huku akifananishwa na kiungo wa zamani wa Uholanzi Edgar Devis.

www.bantuz.com

0 comments:

Post a Comment