Facebook

Tuesday 26 January 2016

KLABU YA MARSEILLE YAPELEKA OFA KWA MBWANA SAMATTA.

Klabu ya Olympique Marseille inayoshiriki Ligi kuu Nchini Ufarasansa (Ligue 1) imeripotiwa kupeleka ofa kwa klabu ya TP Mazembe kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji hatari Mbwana Samatta ambaye alinyakua tuzo mchezaji bora wa ndani wa Afrika mwezi uliopita.

Katika hali ya sintofahamu iliripotiwa Samatta kusaini mkataba wa awali na klabu ya Genk inayoshiriki ligi kuu nchini Ubelgiji na utata uliojitojeza ni Klabu ya TP Mazembe kuweka vipengele vigumu kwa klabu ya Genk katika makubaliano ya kumsajili mchezaji huyo hali iliyopelekea dili la Samatta aliyebakiza muda wa miezi miwili katika mkataba wake kushindikana.

Hapo awali klabu nyingine ya Ufaransa ya Nantes ilituma maombi ya kumsajili Samatta dili likashindikana lakini hivi sasa Kama dili ka Genk halitokamilika Samatta anapendelea kwenda Kusini mwa Ufaransa kujiunga na miamba ya soka nchini humo Klabu ya Marseille.

Endelea kutembelea www.bantuz.com kupata habari za kina na uhakika.

0 comments:

Post a Comment