Facebook

Friday 29 January 2016

Mbwana Samatta asajiliwa rasmi na klabu ya KRC GENK ya nchini Ubelgiji.

Mshambuliaji hatari Mbwana Ally Samatta 'Popa' ambaye aliibuka mfungaji bora katika michuano ya klabu bingwa barani Afrika na kisha kujinyakulia Tuzo ya Mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza Afrika.Amekamilisha usajili wake akitokea klabu ya TP Mazembe ya nchinI DR Congo.

Dili la Sammata kujiunga na miamba ya soka ya Nchini Ubelgiji,KRC Genk limekamilika mara baada ya mmiliki wa klabu ya TP Mazembe hapo juzi kumruhusu Sammata kijiunga na klabu hiyo.

Sammata amesaini mkataba wa miaka 4 itakayomfanya kukipiga katika klabu hiyo mpaka 2020 huku akikabidhiwa jezi namba 77.

Klabu ya KRC Genk kupitia website yake na ukurasa wake wa twitter wamedhibitisha dili hili kukamilika na kuanzia hivi sasa Sammata atakuwa mchezaji halali wa Klabu ya KRC Genk na kufungua njia kwa wachezaji wengine kwenda kukipiga huko barani Ulaya.

0 comments:

Post a Comment