Facebook

Monday 18 January 2016

Man United yapata ushindi mwembamba nyumbani kwa Liverpool.

Wayne Rooney alifunga bao lake la kwanza katika uwanja wa Anfield tangu mwaka 2005 na kuiwezesha timu yake kupanda katika msimamo wa ligi ya Uingereza.

Liverpool ilitawala mchezo huo huku mkwaju wa Emre Can ukipanguliwa na kipa David De Gea.Lakini Liverpool walilazimika kulipa makosa yao wakati Wayne Rooney alipofunga mkwaju mzuri akiwa karibu na eneo la hatari baada ya kichwa cha Marouane Fellaini kugonga mwamba wa goli.

Wageni hao ambao sasa wako katika nafasi ya tano walikuwa hawajashambulia hata mkwaju mmoja katika lango la Liverpool hadi mshambuliaji huyo wa Uingereza alipofunga bao hilo la ushindi.Liverpool itasalia katika nafasi ya tisa ikiwa alama sita nyuma ya Manchester United.

0 comments:

Post a Comment