Facebook

Thursday, 24 April 2014

"Class of 92" kuiongoza Manchester United.........


CLASS_OF_92 

JUMAMOSI Old Trafford itashuhudia Historia mpya wakati Wachezaji wao Nguli, Ryan Giggs, Nicky Butt, Phil Neville na Paul Scholes, watakapoiongoza Timu wakiwa Benchi la Ufundi kwenye Mechi ya Ligi Kuu England dhidi ya Norwich City.
Mechi hii, ambayo sasa imeleta mvuto mkubwa, pia itashuhudiwa na Famila ya Glazer, Wamiliki wa Man United, ambao Leo hii wametua Manchester kufuatilia mchakato wa Meneja mpya.
Mara baada ya David Moyes kufukuzwa kazi Juzi Jumanne na Ryan Giggs kuteuliwa kama Meneja wa Muda, Giggs aliwaita wenzake Nicky Butt, Phil Neville na Paul Scholes kukaa nae Benchi kumsaidia kuiongoza Man United kwenye Mechi zao 4 za Ligi zilizobaki.
Wachezaji hao, pamoja na David Beckham na Gary Neville, ndio waliounda Kikosi maalum cha Man United cha Wachezaji Chipukizi kilicholeta mafanikio makubwa na kubatizwa ‘CLASS OF 92’ ikiashiria Mwaka walioibukia kuichezea Timu ya Kwanza ya Man United.
Habari za ndani ya Old Trafford zinasema kuwa mara baada ya Ryan Giggs kuteuliwa Meneja, aliwaambia Wachezaji wakati umefika wa kurudi kucheza kama Manchester United, kushambulia bila kuogopa Timu na kuzibana Timu bila kujali wao ni nani.
Nae Nicky Butt, ambae ndie alikuwa Kocha wa Timu ya Rizevu ya Man United, ameiambia MUTV, Kituo cha TV cha Man United, kuhusu Mechi yao na Norwich City kwamba: “Hii ni Gemu kubwa kwetu na fahari kubwa kwetu. Kuwa pamoja ni kitu kisichoaminika. Tuliingia hapa pamoja tukiwa na Miaka 12 na kwa sisi kuwa pamoja sasa ni fahari kubwa mno!”
Butt alisisitiza kuwa Man United inao Wachezaji wazuri mno ambao wanaijali Timu yao na wanaitakia mema Klabu yao.

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment