Facebook

Thursday, 24 April 2014

Meya wa kwanza mwanamke kuongoza Paris..............


Anne Hidalgo, mwenye skafu nyekundu na nyeupe akifurahia ushindi  alioupata katika uchaguzi wa jumapili
 
Anne Hidalgo, mwenye skafu nyekundu na nyeupe akifurahia ushindi alioupata katika uchaguzi wa jumapili
Paris inapata meya wake wa kwanza mwanamke lakini chama chake tawala cha Socialistics kilipata kipigo katika mzunguko wa pili wa uchaguzi wa serikali za mitaa nchini Ufaransa.

Anne Hidalgo mzaliwa wa Spain alimshinda mpinzani wake m-conservative kushinda wadhifa wa cheo cha juu katika mji mkuu wa Ufaransa.

Hidalgo awali alihudumu kama naibu wa meya anayemaliza muda wake, Betrand Delanoe. Alishinda kwa ahadi ya kujenga nyumba mpya za umma na kurahisisha zaidi mfumo wa huduma ya kulea watoto kwa familia za Paris.


Waangalizi wengi wa kisiasa wanaiangalia ofisi ya meya wa Paris kama hatua moja kusonga mbele kwa urais wa Ufaransa.


Lakini chama cha Hilalgo cha Socialists hakikufanya vyema katika miji na miji mikubwa mingi mingine ya Ufaransa,  imepoteza uungaji mkono kwa wanaopinga uhamiaji na wanaopinga chama cha European Union national Front.


Uchaguzi unaonekana kama kura ya maoni kwa rais asiye maarufu, Francois Hollande.
Wapiga kura wamekasirishwa na kudorora kwa uchumi na kiwango cha juu cha ukosefu wa ajira

Related Posts:

  • Mama anayeugua Ebola atoroshwa Mwanamke aliyeambukizwa Ebola atoroshwa Hospitalini huko Freetown Hali ya Tahadhari imetangazwa mjini Freetown Sierra Leone baada ya mwanamke mmoja aliyeambukizwa Ebola kutoroshwa kutoka Hospitalini na jamaa zake kw… Read More
  • Juhudi za kutafuta amani Gaza zaingia dosari. Wapalestina zaidi ya 800 wameuawa na Waisraeli 35 Israeli imeendelea kuivirumishia makombora Gaza kucha kutwa ,huku kikao cha mawaziri wa baraza la Usalama kikitarajiwa huko Marekani kujadili mapendekezo mapya ya … Read More
  • Maandamano yazuka Palestina polisi wakabiliana na raia Palestina Maandamano makubwa yamefanyika katika ukingo wa Magharibi mwa Palestina karibu na mpaka wake na Israel kupinga mashambulio yanayofanywa na Israel. Waandamanaji hao wakiwa na hasi… Read More
  • Air Algerie AH5017: Abiria wote waliaga Abiria wote wa ndege ya Air Algerie waliangamia jangwani Abiria wote na wahudumu wa ndege ya Air Algerie AH5017 waliangamia jangwani. Rais wa Ufaransa Francois Hollande ametangaza kuwa majeshi … Read More
  • Mabaki ya ndege Algeria yaonekana Mabaki ya ndege iliyopotea ikiwa na watu 116 njiani kutoka Burkanafaso kwenda Algers yamepatikana nchini Mali. Maafisa wa Jeshi wa Burkina faso wamesema ndege hiyo iliyokuwa chini ya shirika la ndege la Algeria imeang… Read More

0 comments:

Post a Comment