Facebook

  • Tutorial 1

    This is Trial

  • Tutorial 2

    This is slide 2 description. Go to Edit HTML and replace these sentences with your own words. This is a Blogger template by Lasantha - PremiumBloggerTemplates.com...

  • Tutorial 3

    This is slide 3 description. Go to Edit HTML and replace these sentences with your own words. This is a Blogger template by Lasantha - PremiumBloggerTemplates.com...

Sunday, 22 March 2015

BAADA YA ZITTO KABWE,AFANDE SELE AJIUNGA RASMI ACT TANZANIA.

Baada ya hapo jana aliyekuwa mwanachama wa CHADEMA Zitto Zubery Kabwe kuhamia chama cha ACT TANZANIA.

Leo hii aliyekuwa mwanachama wa CHADEMA, msanii maarufu na Mfalme wa Rhymes Tanzania Afande Sele amehama rasmi CHADEMA na kuamua kuungana na Zitto Kabwe baada ya kutangaza rasmi kujiunga na chama cha ACT TANZANIA.

BAADA YA ZITTO KABWE,AFANDE SELE NAE AJIUNGA RASMI ACT TANZANIA.

Baada ya hapo jana aliyekuwa mwanachama wa CHADEMA Zitto Zubery Kabwe kuhamia chama cha ACT TANZANIA.

Leo hii aliyekuwa mwanachama wa CHADEMA, msanii maarufu na Mfalme wa Rhymes Tanzania Afande Sele amehama rasmi CHADEMA na kuamua kuungana na Zitto Kabwe baada ya kutangaza rasmi kujiunga na chama cha ACT TANZANIA.

UCHAMBUZI WA MECHI KALI ZA LEO LIGI KUU UINGEREZA NA Mr CHOI (KWA TAARIFA YAKO)

LIVERPOOL vs MAN UTD
   Licha ya timu zote kutokuwa katika mbio za ubingwa huku mbio zao zikiwa kuwania nafasi ya nne ili kucheza kombe la mabingwa Ulaya bado historia inafanya mchezo huu kuwa na mvuto wa kipekee.

   Utawala wa Liver kwenye miaka ya 1975/90  huku wakichukua vikombe vya ligi kuu 18 ulivunjwa na Man Utd ambao waliibuka miaka ya 1993/13 kwenye kuchukua vikombe vya ligi na mpaka sasa wana vikombe 20.
   Ni sehemu moja tu ambayo bado Liver wanatawala kwa wingi wa vikombe napo ni ktk Uefa wakiwa wamechukua mara 5 huku Man Utd wakinyakua mara 3. Katika makabati ya timu zote Man Utd bado ni kinara wa vikombe wakiwa na idadi ya vikombe 55 dhidi ya 48 vya Liverpool.
   Ushindi wa Liverpool leo utakuwa wa 58 mbele ya Utd walioshinda mara 68 huku wakitafuta ushindi wa 69 na timu hizi zimetoka sare mara 44.
     Liverpool wapo nafasi tano wakiwa na pointi 54 wamekuwa na matokeo mazuri kwa kipindi cha hivi karibuni na endapo watashinda leo watafikisha michezo 14 pasipo kupoteza. Gerrard amekuwa na mchezo mzuri pindi akikutana na Man Utd huku akifunga mara 7 kati ya 11 kwenye mechi za Ligi.
    Henderson ambaye ameonekana kuvaa viatu vya Gerrard vyema atakuwa katika safu ya kiungo pamoja na Allen kupambana na Herrera pamoja na Carrick kama Van Gaal atamchezesha kati. Kwa ujumla vikosi vyote havita kuwa tofauti sana kutoka michezo waliocheza hivi karibuni.
   Licha kucheza vibaya kwenye mchezo wa awamu ya kwanza na kufungwa goli 3 Mignolet kwa sasa yupo ktk ubora mzuri akichagizwa na safu yake ya ulinzi inayocheza vyema.
    Man Utd wao wapo nafasi ya nne kwa pointi 56 ni timu pekee iliopata ushindi mara nyingi pale Anfield kuliko timu nyingine za ligi kwa hivi karibuni wanamichezo migumu hivyo mahesabu yalianza kwa Spurs na wanahitaji muendelezo wake licha ya kutokuwa wazuri hasa safu ya ulinzi ambapo De Gea amekuwa akifanya kazi ya ziada hivi sasa tangu Rooney arejeshwe kwenye nafasi yake ya ushambuliaji ameonesha nini hasa Man Utd wanastaili fanya na hii leo ata tafuta goli la 170 katika ligi.
   Mwamuzi wa mchezo huu ni Martin Aikison alie chezesha michezo 24 mpaka sasa huku akitoa kadi za njano 96 na nyekundu 5 na kwa aina ya ushindani uliopo wa timu hizi pengine atafikisha kadi 100 kwenye mchezo wake wa 25.

--------- 
HULL vs CHELSEA
     Ushindi wa Man City na Arsenal siku ya jana utawalazimu Chelsea kuibuka na ushindi leo ili kujipa matumaini makubwa ya kuchuku ubingwa wa ligi.
   Ukitizama mchezo wa Soton wiki iliopita walicheza vyema hasa kipindi cha pili mara baada ya kuingia Ramires ambapo Matic hakuwa vyema kwenye mchezo huo, mchezo wa leo kikosi ni kilekile hakito badilika labda upande wa golini na kuanza kwa Willian badala ya Oscar.
   Hull City wao watajaribu kuwa simamisha Chelsea ambapo wanatakiwa kuongeza gepu la pointi kati yao na timu zilizo mkiani mwa ligi. Hawana matokeo mazuri mbele ya Chelsea kwani katika michezo 11 ya karibuni wamefungwa mara 9 na kutoa sare 2.
   Kiungo Huddlestone hatokuwepo kutokana na kadi nyekundu aliopata kwenye mchezo wa Leicester pia Jelaviç atakosa mchezo huu kutokana na majeraha yatakayo muweka nnje wiki 6
   Hull wazuri kujilinda na mara nyingi Bruce amekuwa hafunguki sana pindi akicheza na timu kubwa huku timu yake ikishika nafasi ya pili kwa wingi wa kadi nyekundu ( 5 ) wakiongozwa na Aston Villa (6) . Mchezo utakuwa wa upande mmoja lakini tutaraji mashambulizi ya kustukiza kwa Hull watakao ongozwa na N'doye.

NB:  Hazard ametengeneza nafasi 79 kati ya 74 za Fabregas za kufunga.
  
For more/ Ushauri::
Choikangta.ckt@gmail.com

ZITTO KWABWE AJIUNGA RASMI ACT,AKABIDHIWA KADI No.007194

Baada ya songombingo lililochukua taswira mbalimbali katika jamii kati ya Zitto Kabwe na kilichokuwa Chama Chake CHADEMA.

Hatimaye Zitto Kabwe baada ya Kujiengua CHADEMA amejiunga rasmi na chama cha ACT ambapo anaenda kuungana na Prof Kitila.

Saturday, 21 March 2015

Kenya:Binti wa miaka kumi(10) ajifungua mtoto wa kiume

GLADYS CHELAGAT.AKIWA NA MTOTO WAKE.
Wakati wanaharakati mbali mbali duniani wakipambana kupinga ukatili kwa watoto, huko nchini Kenya mtoto wa miaka 10 ambaye angetakiwa kuwa shuleni akisoma na kucheza na wenzake michezo mbali mbali, anapata jukumu la kumlea mtoto mwenzake. 

Gladys chelagat, anakuwa mama mdogo kabisa duniani baada ya kujifungua mtoto wa kiume jumamosi iliyopita akiwa na umri wa miaka kumi tu (10).

Mtoto huyu alijifungua mtoto wake wa kiume mwenye uzito wa kg 2.8 katika hospital ya kericho nchini kenya.

Hata hivyo Mungu ni mkubwa  kwani pamoja na udogo wa mtoto huyu alijifungua salama bila ya kupata tatizo lolote la kiafya.

HAPPYBIRTHDAY NABII WA SOKA;HAPPYBIRTHDAY RONALDINHO GAUCHO.

Happy Birthday Mwalimu wa Waalimu
mnamo tarehe 21 ya mwezi wa 3 mwaka 1980
huko Port Alegre nchini Brazil, alizaliwa
mfalme wa Soka.

Ujio wake ulitarajiwa, kwani ishara nyingi
zilishajionesha kuwa mbarikiwa atakaekuja
kutambulisha skills zinazopatikana katika ligi
yu karibu kuzaliwa.

kuzaliwa na kukua kwake kulikuwa ni kwa
kibinaadamu zaidi na alisoma na kupata malezi
kama watoto wengine mpaka alipotimiza miaka
13 ndipo matendo ya kinabii yakaanza kuonekana.

Akiwa na umri huo Dinho aliisaidia timu yake
ya mtaa kupata ushindi wa goli 23-0 magoli
ambayo yote aliyatupia yeye.

Huyu ndiye Ronaldo de Assis Moreirra
almaarufu kama Ronaldinho Gaucho-The saint
ambae akiwa uwanjani basi Malaika huacha
shughuli zao na kuanza kumtazama.

Alipofika ulaya alitua katika timu ya Paris Saint
German  ya huko Ufaransa ambapo matendo ya kimiujiza awapo uwanjani yalizivutia klabu nyiingi sana barani humo.

Nilikuwa niko darasa la 3 huko Ukonga-DSM,nakumbuka zilikuwa ni fainali za Kombe la dunia mwaka 2002 zilipigwa huko Korea Kusini na Japan.

Sikukosa mechi hata moja ambayo Brazil walikuwa wanacheza.Kwani sikupenda kukosa kuiona miujiza ya Ronaldinho Gaucho.

Huyu ndiye Gaucho aliyemfanya Kocha wa Brazil enzi hizo Luis Philipe Scoral amteme Gwiji wa soka wa Brazil wakati huo Romario kwa utovu wa Nidhamu,dunia nzima,waBrazil hadi rais wa Brazil alimshangaa kwa kumtema Romario.

Lakini Scorali alikuja kuibuka na kijana kutoka PSG Ronaldinho Gaucho na kufanikiwa kulichukua kombe hilo huku Goli la maajabu zaidi linakumbukwa ni lile la Robo fainali baina ya Brazil dhidi ya Uingereza,Dinho alipiga faulo ya ajabu iliyomshinda David Siemen na kujaa wavuni.

Hakudumu sana na PSG kwani  Klabu za Manchester United na Barcelona zilimuwinda kwa udi na uvumba.

Lakini Barcelona ndio walikuwa katika mipango ya kuijenga timu yao.Pesa walikuwa nayo, uwanja walikuwa nao, ila kuna kitu wakawa wamekosa.Na hapa sasa ndipo ikawalazimu wamchukue
mtu atakaekuja kufanikisha kuiunda na kuipa
mafanikio.

Na ndipo msemo wa ;DINHO MADE BARCA AND
BARCA MADE MESSI ulipotokea.Hatimae Dinho akatua Nou Camp nou na kuanza ujenzi wa timu.
Barca ikawa timu ya ushindani badala ya
ushiriki..

Barcelona ikaanza kupata ushindi mfululizo katika mashindano yote, barca ikaanza kujaza uwanja kwani habari za miujiza ya soka anayofanya Saint Gaucho zilitapakaa ulimwenguni kote
mfalme Ronaldinho alitibu kiu za wote
waliokuwa na njaa ya kuuona ufundi wa mpira

Mfalme huyu hakujaliwa kukasirika kabisa.Anakupiga vyenga ukimkata anacheka tuuu.
Ronaldinho hakuleta mataji tu bali alijengea
heshima ambayo kamwe haiwezi futika
machoni mwa waliomuona ilifika hadi hatua
mashabiki kutoka timu yenye upinzani wa
damu na nyama na barca "real madrid' kiasi
cha kupewa standing ovation akiwa uwanja wa
santiago bernabeu.

kitu ambacho ni adimu kwa mchezaji wa barca kufanyiwa.Kama uliwahi guswa na miujiza ya "Ronaldinho Gaucho "tuungane kumtakia heri ya kuzaliwa na maisha marefu zaidi...
Wote tuseme Happy birthday "ronaldinho"

-katemi Methsela.

'HOUSE GIRL' ASABABISHA KIFO, VIJANA WA KAMASAI "MORANI" WACHOMA NYUMBA KULIPIZA KISASI ARUSHA

Makundi ya vijana wanaosadikiwa kuwa ni wa jamii ya kimaasai
maarufu kama “Morani” katika eneo la Olasiti Jijini Arusha,
wameteketeza kwa moto mali mbalimbali zikiwemo nyumba pamoja na
magari ya wakazi wawili wa eneo hilo, wanaotuhumiwa kumpiga na
kumsababishia kifo kijana mmoja wa jamii hiyo.
Kijana Melita John anadaiwa kuuawa na Bernard Kavishe mkazi wa
Olasiti akishirikiana na majirani zake wawili akimtuhumu kijana huyo
kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na msichana wake wa kazi za ndani
ambaye ni binti wa miaka 17 anayefahamika kwa jina la Monica
Emanuel.

Taarifa zaidi zinadai kuwa hatua ya morani wa kimaasai kujichukulia
sheria mkononi na kuteketeza nyumba na magari pamoja na mali
nyingine za watuhumiwa hao ni katika kulipiza kisasi kutokana na kifo
cha mwenzao wanayedai hakuwa na hatia.
Inadaiwa mtuhumiwa wa kwanza wa mauaji hayo Benard Kavishe
baada ya kuwasili nyumbani kwake majira ya saa saba mchana na
kugonga gate la nyumbani kwake ilimchukua muda wa dakika kumi
msichana wake wa kazi kufungua ndipo alipoingia ndani na kumkuta
kijana Melita akiwa bila nguo ndipo alipowaita majirani wenzake na
kumshambulia kwa kipigo hadi kumsababishia mauti
Jeshi la Polisi kupitia wa Kaimu kamanda wa Mkoa wa Arusha
Kamishna Msaidizi Edward Balele akithibitisha tukio hilo amesema
baada ya watuhumiwa wanaosadikiwa kushiriki katika mauaji ya
kijana Melita wanashikiliwa kwa mahojiano zaidi..

Huduma ya Taxi yapigwa marufuku Ujerumani.

Ni wiki ngumu ya Uber.Mahakama moja nchini Ujerumani imepiga
marufuku huduma ya bei nafuu ya texi ya Uberpop baada ya
kuamua kwamba inaenda kinyume na sheria za uchukuzi.

Vilevile afisi
za kampuni hiyo zilizopo mjini Paris zimevamiwa na maafisa wa polisi
wa Ufaransa wanaochunguza huduma hiyo ya Uberpop,huku watu 30
wanaohusishwa na kampuni hiyo wakishtakiwa kwa kuendesha kampuni
hiyo ya texi nchini Korea Kusini bila vibali.Uber imesema kuwa
wafanyikazi wake wa koreakusini hawajavunja sheria na kuutaja
uvamizi huo wa Paris kama usio wa haki.