Facebook

Monday 5 October 2015

MAONI NA POLE MITANDAONI-KIFO CHA MCH. MTIKILA!

-Mwigulu Nchemba.
Nimesikitishwa na taarifa za kifo cha mwanasiasa nguli Mch. Christopher Mtikila. Tumepata pigo kama taifa, tuungane kumuombea apumzike kwa amani.

-Malisa Godlisten.
Buriani Mch. Mtikila. Hatima ya maisha yetu ipo mikononi mwa Mungu pekee. Tusiwadhihaki wagonjwa bali tuwaombee maana hakuna ajuaye kesho yake. However, tunakuombea upumzike kwa amani.

-Manawa M. Bukwimba.
Waliosema Lowasa ni mgonjwa sijui maiti inayotembea, wameanza kuwa maiti wao. Mwingine kafariki leo kwa ajali na wanayemwita maiti anaendelea na maisha yake ya kawaida. Ugonjwa na uzima ni kudra toka kwa Allah. MUNGU NI MWEMA SANA.

-Bob Chacha Wangwe.
Ni dhahiri kuwa Tanzania imepoteza mtu muhimu sana. Pamoja na mapungufu ya kibinadamu, Mchango wa Rev Chritopher Mtikila katika kujenga Demokrasia nchini ni wa MFANO. Nimeumizwa sana na kifo chake. R.I.P!

-Mimi Mwanakijiji.
Harakati za mabadiliko na ukuaji wa demokrasia Tanzania zimepata pigo kubwa leo hii. Habari za kifo cha mpigania haki za raia na binadamu Mchungaji Chritopher Mtikila nimezipokea kwa masikitiko makubwa na mshitiko usio na kifani.

-Joyce Kiria.
May yo soul Rest in eternal peace Mchungaji Mtikila, Bwana ametoa na Bwana ametwaa. Atukuzwe mola wetu na utukufu wake.

-Halima James Mdee.
R I P Rev. Mtikila. Pole kwa familia, pole kwa wanachama na wapenzi wako. Bwana Ametoa, Bwana ametwaa.

-Philipo Mwakibinga.
Kwasababu ya rangi zao za Bendera! Kwasababu ya mihemko yao ya uchaguzi, watakupuuza na kukupeza. Mimi nitakukumbuka Daima kwa uzalendo wako juu ya Taifa letu na hasa asili yetu na hasa asili yetu watanganyika. R. I. P Mtikila.

-Shy-Rose Bhanji.
Mungu akulaze pema Mchungaji Mtikila.... Hakika duniani tunapita tu.

-John Mnyika.
Pole sana kwa familia, ndugu, jamaa na wote walioguswa na kuondokewa  Mwenyekiti wa DP Mch. Mtikila. Mungu amjalie kuionja mbingu yake.

************************************

0 comments:

Post a Comment