Facebook

Sunday 4 October 2015

Mwanasiasa mkongwe, Mchungaji Christopher Mtikila afariki dunia kwa ajali ya gari asubuhi ya leo.

Mwanasiasa mkongwe, Mwenyekiti wa chama cha kisiasa cha DP na Mtumishi wa Mungu, Mchungaji Christopher Mtikila amefariki kwenye ajali ya gari asubuhi ya leo.

Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani, Jafari Mohamed, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa "Taarifa za mwanzo" zinasema amefariki saa 12 kasorobo asubuhi katika kijiji cha Msolwa, Chalinze.

Amesema gari lililokuwa limempakia lilikuwa linatokea Morogoro na kwamba walikuwa watu wanne ambapo wengine watatu wamejeruhiwa vibaya.

Majeruhi wamekimbizwa katika Hospitali ya Tumbi.

Bwana ametoa na Bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe.

MWENYEZI MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU CHRISTOPHER MTIKILA. AMEN.

0 comments:

Post a Comment