Facebook

Sunday, 15 June 2014

Uingereza yanyamazishwa na Italy

Mabingwa wa zamani wa kombe la dunia Italy imeanza vyema kampeni yake ya kuwania kombe la dunia nchini Brazil baada ya kuichapa Uingereza mabao mawili kwa moja katika mechi kali.
Bao la ushindi la Italy lilifungwa kwa kichwa kupitia mshambuliaji matata Mario Baloteli mda mchache tu baada ya kipindi cha mapumziko.
Awali mshambuliaji wa Liverpool Daniel Sturridge alikuwa amekomboa bao lililofungwa na Claudio Marchisio wa Italy.
Mechi hiyo ilichezwa chini ya viwango vya juu vya joto katika uwanja wa Manaus uliopo katikati ya msitu wa Amazon.
Katika mechi za awali ,Costa Rica ilitoka nyuma na kuishinda Uruguay mabao matatu kwa moja huku Colombia nayo ikiicharaza Ugiriki mabao matatu bila katika mji wa Belo Horizonte.
Wakati huohuo miamba ya soka barani afrika Ivory Coast imeimarisha matumaini ya bara hili baada ya kutoka nyuma na kuishinda Japan kwa mabao mawili kwa sufuri.
Ivory Coast ilijipatia mabao yake kupitia wachezaji Wilfried Bony na aliyekuwa mchezaji wa Arsena Gervinho huku Japan ikifunga kupitia mshambuliaji wake keisuke Honda.


Hivi sasa tunahamia katika site yetu mpya inayoitwa www.bantutz.com ni katika kuboresha huduma zetu za kutoa habari za uhakika na burudani.

Related Posts:

  • Webb huenda akachezesha fainali Brazil Refa muingereza anayefahamika kwa ukakamavu wake Howard Webb ni miongoni mwa waamuzi 15 walioteuliwa kusalia Brazil kushiriki mechi zilizosalia za kombe la dunia. Webb mwenye umri wa miaka 42 ni miongoni mwa w… Read More
  • Afisa wa Match Hospitality akamatwa Maafisa wa polisi nchini Brazil wamemkamata afisa mkuu mtendaji wa kampuni mshirika wa FIFA kwa tuhuma za uuzaji tiketi za kombe la dun… Read More
  • BRAZIL YAPOKEA KIPIGO CHA MBWA MWIZI  -Brazil yapokea kichapo cha Mbwa mwizi katika mchezo wao wa jana na Ujerumani baada ya kutandikwa bao 7 huku wao wakiambulia bao 1 walilofunga dakika za majeruhi. - Huzuni ilitanda kwa mashabiki wa Timu ya Brazi… Read More
  • Van Persie hatihati kuwakosa Argentina. Mshambuliaji wa Uholanzi na Manchester United,Robin Van Persie anasumbuliwa na ugonjwa wa tumbo kwenye kambi ya timu ya taifa. Ni masaa 24 yamebaki ili wacheze na Argentina kwenye nusu fainali. Madaktari wanajitahidi kuf… Read More
  • Luiz "Tuwieni radhi Ujeruman ni timu bora" Luiz akilia baada ya kushindwa na Ujerumani Nahodha wa muda wa Brazil David Luiz amewataka mashabiki wa tim,u hiyo kote duniani kuwasamehe wachezaji w… Read More

0 comments:

Post a Comment