Facebook

Monday 16 November 2015

Diamond Platnumz na Vanessa Mdee washinda tuzo 4 za AFRIMA 2015 Nigeria

Tuzo za All Afrika Music Awards 2015 (AFRIMA) zimetolewa usiku wa Jumapili November 15 jijini Lagos, Nigeria ambapo Tanzania imetoa washindi wawili.

Diamond Platnumz aliyekuwa akiwania tuzo hizo ameibuka mshindi wa vipengele 3 kikiwemo kipengele muhimu cha Msanii Bora Wa Mwaka (Artist Of The Year) ambayo ilikuwa ikiwaniwa na Alikiba, Davido, Jose Chameleone, Wizkid, Yemi Alade, Sarkodie na Flavour.Vipengele vingine alivyoshinda Diamond ni Msanii Bora wa Kiume Afrika Mashariki (Best Male Artist in Eastern Africa) pamoja na Wimbo Bora Afrika (Nasema Nawe)


Vanessa Mdee ameshinda kipengele cha ‘Best African Pop’ kupitia wimbo wake ‘Hawajui’.
msanii mwingine kutoka Tanzania 
aliewania tuzo hiyo 
Ni Linah ambae alikua kwenye kipengere cha msanii bora wa kike wa Afrika Mashariki

0 comments:

Post a Comment