Klabu ya Lille inayoshiriki Ligi Kuu ya Ufaransa imewasilisha rasmi ofa ya kumsajili mshambuliaji wa TP Mazembe ya DRC) na Taifa Stars, imefahamika.
Katika mahojiano na moja ya vituo vya televisheni vya Afrika Kusini usiku wa kuamkia jana, Mmiliki wa TP Mazembe, Moise Katumbi, alisema klabu hiyo imewasilisha maombi hayo na sasa wanasubiri kuitwa kwa ajili ya kufanya mazungumzo.
Katumbi alisema Lille ndiyo klabu ambayo imekuwa ikikumbushia maombi yake mara kwa mara tofauti na klabu nyingine zilizowasilisha maombi ya kumnasa straika huyo ambazo hata hivyo, hakuwa tayari kuzitaja.
Meneja wa Samatta, Jamal Kisongo, pia alikiri kufahamishwa juu ya ofa ya Lille na kueleza kuwa waliamua kusimamisha mazungumzo kuzipa kipaumbele mechi mbili za fainali ya Klabu Bingwa Afrika dhidi ya USM Algiers ambazo TP Mazembe walishinda zote na kutwaa ubingwa.
"Hiyo ofa ninaijua, ilikuwa mapema na tulikubaliana mjadala wake uanze baada ya mechi za fainali kumalizika, wakati wowote tunaweza kukutana nao kwa ajili ya kuijadili," alisema meneja huyo.
Kisongo aliongeza kuwa hawatakuwa na papara katika kufanya uamuzi kwa sababu mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 22 yuko katika kiwango cha hali ya juu kwa sasa.
Alipotafutwa na mtandao huu wa
Bantuz jana kuzungumzia masuala ya usajili, Samatta alisema atakuwa tayari kuanza kuzungumzia mahali anapokwenda baada ya kuitumikia nchi (Taifa Stars) katika mechi mbili zinazoikabili dhidi ya Algeria.
Friday, 13 November 2015
Klabu ya Lille yawasilisha rasmi ofa ya kumsajili Samatta.
Related Posts:
Kerr : Kumbe Simba SC walinidanganya kuhusu MgamboTanga. Kocha wa Simba, Dylan Kerr amefichua siri ambayo ni vigumu kuiamini. Alisema alilazimika juzi kupanga viungo wengi dhidi ya Mgambo JKT kutokana na kupewa taarifa kuwa timu hiyo inacheza soka la kushambulia kwa wakati w… Read More
Wenger akataa kuzungumzia suala la yeye kushikana mkono na Mourinho.Arsene Wenger leo amegoma kuweka wazi kama atapeana mkono na Jose Mourinho lakini ameweka kando juu ya umuhimu wa uhusiano wao kutokwenda vizuri kuelekea ziara ya Arsenal kwenda kuwatembelea Chelsea. Mameneja hao wawili walio… Read More
Huyu ndiye Mahrez anayempa jeuri kocha wa Leicester City na Kuwanyima Usingizi mabeki Ligi Kuu Uingereza Claudio Ranieri ameanza kutajwa sana kama Meneja aliyerejea kwa kasi kwenye EPL na kuanza kutishia uhai wa timu ndogo ambazo ziliamini Leicester City na Sunderland ndio wahanga wa kuteremka daraja hivo wao hawatokuwa na shaka… Read More
Ratiba ya Mechi za Ligi kuu Uingereza Septemba 19 na 20.Kesho Jumamosi Septemba 19 14:45 Chelsea vs Arsenal 17:00 Aston Villa vs West Brom 17:00 Bournemouth vs Sunderland 17:00 Newcastle Utd vs Watford 17:00 Stoke City vs Leicester 17:00 Swansea vs Everton 19:30 Manchester City vs… Read More
NINACHOKIAMINI MAESTRO:UCHAMBUZI CHELSEA vs ARSENAL. Na: Ayoub Hinjo (Ayo's Mata Maestro). CHELSEA vs ARSENAL 1: ULINZI CHELSEA: Chelsea ndio timu iliyoruhusu magoli mengi kwenye ligi kuu kuliko timu yoyote(Magoli 12). Hii inaonyesha ni jinsi gani ukuta wa Chelsea umeku… Read More
0 comments:
Post a Comment