Facebook

Saturday 17 January 2015

TETESI ZA SOKA ULAYA- DIRISHA DOGO LA USAJILI


Meneja wa Manchester City Manuel Pellegrini amesema yuko tayari kutoa pauni milioni 480 kumnunua mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi, 27 (Sun),

 Arsenal wameanza mazungumzo na Borussia Dortmund ya mkataba wa pauni milioni 63 kuwasajili kiungo Ilkay Gundogan, 24, na beki wa kati Mats Hummels, 26 (Star),

Palermo wamesema wamekataa dau kutoka Manchester United la kutaka kumsajili mshambuliaji kutoka Argentina Paulo Dyabala, 21 (Guardian), 

Paris St-Germain, Porto na Juventus wanamnyatia Adnan Januzaj, 19 wa Manchester United kumchukua kwa mkopo (Sun), 

Crystal Palace wanakaribia kumsajili mshambuliaji wa Swansea Bafetimbi Gomis, 29 (Times), 

Meneja wa West Brom Tony Pulis wanamtaka kiungo wa Manchester United Darren Fletcher (Express na Star), 

Swansea wanataka kutumia fedha za mauzo ya Bony kumnunua kiungo wa Stuttgart Alexandru Maxim, 24 (Telegraph), 

Manchester United wameanza mazungumzo na PSG ya kumsajili beki kutoka Brazil Marquinhos, 20 kwa pauni milioni 30 (Le10sport), 

Meneja wa Jose Mourinho yuko tayari kuwauza Andre Shurrle, 24 na Mohamed Salah, 22 ili kumsajili beki wa Real Madrid Raphael Varane, 21 (Star).

0 comments:

Post a Comment