Facebook

Saturday, 17 January 2015

Cameroon kupambana na Boko Haram

 
Serikali ya Cameroon imesema Chad itatuma kikosi kikubwa cha wanajeshi wake kupambana na wapiganaji wa kiisilamu wa Boko Haram mpakani mwa Nigeria na nchi hio.
Tangazo hili limetolewa siku moja baada ya Chad kusema kwamba itaunga mkono jirani yake Nigeria katika harakati dhidi ya wapiganaji wa kiisilamu wa Boko Haram.

Hakuna taarifa zozote zimetolewa kuhusu idadi kamili ya wanajeshi watakaopelekwa huko au siku.
Mnamo siku ya Jumanne, Cameroon ilisema kwamba iliwaua wapiganaji 143 wa Boko Haram, ambao walishambulia kambi zake katika eneo la Kolofata karibu na mpaka na Nigeria.
Ilisema kuwa mwanajeshi mmoja alifariki wakati wa mashambulizi hayo ambayo yalisababisha ufyatulianaji risasi mkali kati ya wanajeshi na waasi hao kwa muda wa saa tano.

lilikuwa shambulizi la kwanza kubwa kufanywa na Boko Haram dhidi ya Cameroon tangu kundi hilo kutishia kiongozi wa nchi hio katika kanda ya video waliyoiweka kwenye mtandao mapema mwezi huu.
Wanamgambo hao wameteka miji na vijiji kadhaa ambavyo wanavidhibiti Kaskazini Mashariki mwa Nigeria katika harakati zao ambazo wameziendeleza kwa miaka sita sasa.

Related Posts:

  • Mahakama:Pistorius hakukusudia kuuaJaji anayetoa uamuzi katika kesi ya mauaji inayomkabili Oscar Pistorius, amesema upande wa mashitaka umekosa kuthibitishia kikamilifu shitaka kuu la kwanza dhidi ya Pistorius kuwa alikusudia kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp… Read More
  • Binti alazimisha penzi kwa kumshikia Bastola mwanaume.Marekani: Binti (25) akamatwa kwa kosa la kumlazimisha kijana (33) kufanya naye mapenzi akiwa kamshikia bastoka kwenye gari lake baada ya kijana huyo kuomba lift. Inasemekana huyo binti alikuwa na mwanamke mwingine ambaye wal… Read More
  • Nyama ya Kiboko yawaletea maafa Afrika KusiniWatu kumi walikanyagwa na gari lililokuwa linakwenda kwa mwendo wa kasi walipokuwa wanajaribu kujipatia angalau kipande cha nyama ya Kiboko mwishoni mwa wiki. Taarifa hii ni kwa mujibu wa mtandao wa Daily Nation. Kiboko huyo … Read More
  • Mchakato wa katiba kusitishwaKumekuwa na maoni tofauti kufuatia hatua ya kusitisha mchakato wa kura ya maoni ya Katiba Mpya nchini Tanzania. Katika kikao cha Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete na Viongozi wa vyama vya siasa nchini humo wamekubaliana kuwa ku… Read More
  • Miaka 8 jela kwa jaribio la kutaka kumuua mkosoaji wa Rais wa RwandaWatu wanne - Watanzania wawili na Wanyarwanda wawili- waliokutwa na hatia ya kutaka kumuua mkosoaji wa Rais wa Rwanda Paul Kagame nchini Afrika Kusini wamehukumiwa kwenda jela kwa miaka minane kila mmoja. Mkuu wa zamani wa je… Read More

0 comments:

Post a Comment