MENEJA wa kundi la TMK Wanaume Family aliye pia
mkurugenzi wa MKubwa na Wanae, Said Fella
'Mkubwa' amethibitisha kuwa msanii YP amefariki
dunia usiku wa kumakia leo.
Akizungumza na BantuTz hivi punde kwa njia ya simu, Fella
alisema YP amefariki akiwa katika Hospitali ya Temeke na siyo nyumbani kwao kama taarifa za
awali zilizokuwa zimetufikia na kwamba alikuwa
akisumbuliwa na maradhi ya Kifua.
'Ni kweli YP amefariki akiwa Temeke Hospitali
alikokuwa amelazwa kwa siku kadhaa, alikuwa
akisumbuliwa na Kifua, kwa kweli ni pigo kwetu na tasnia nzima ya muziki kwani ni hivi karibuni
tumetoka kumpoteza pia Side Mnyamwezi,"
alisema Fella mmoja wa wadu wa muziki
waliosaidia kukuza muziki wa kizazi kipya kwa
kuibua vipaji kila uchao.
Fella alisema kwa sasa wanasubiri kuwasiliana na ndugu na familia ya marehemu YP kwa ajili ya
kujua mazishi yake yatafanyika lini na wapi, japo
alisema huenda akazikwa leo pande za TMK.
Mwenyezi Mungu Ailaze Roho ya Marehemu Mahali
Pema Peponi.
Tuesday, 21 October 2014
Msanii Y.P wa kundi la TMK Wanaume Family afariki dunia.
Related Posts:
Mungu aliumba Dunia,Da Vinci aliijenga Dunia. Katika dunia ya leo ni wanadamu wengi sana ambao wanakumbukwa kwa matendo yao mbalimbali waliyoyafanya wakiwa hai.Tumefanikiwa kuwakumbuka binadamu mbalimbali ambao waliifanyia dunia mambo makubwa na dunia haitweza kuwasah… Read More
Linex akamatwa na wanajeshi,kisha kavuliwa Nguo. Kitu kama hiki kiliwahi kumtokea mwana-hiphop Young Killer miezi michache iliyopita ambapo alivuliwa nguo ya jeshi aliyokua ameivaa.Wiki kadhaa baadae ikatangazwa tena kwenye vyombo vya habari kwamba ni marufu… Read More
Akon ajikinga na Ebola … Read More
Mwanzilishi wa kampuni ya 'Apple' aliwazuia watoto wake kutumia iPad, iPhone na iPod, fahamu sababuBidhaa za kampuni ya Apple zina mashabiki na wateja wengi duniani, hii inathibitishwa na foleni kubwa ya watu waliojitokeza kwenye vituo mbalimbali duniani kununua toleo jipya la iPhone6. Tumesikia watu wakiachana ama familia… Read More
Mfahamu "Drogba" wa Mbuga ya Selous na jinsi anavyojiingizia kipato. KATIKA kipindi cha miaka minne iliyopita hadi kufikia leo, watalii wanaoenda kutembelea Pori la Akiba la Selous lililopo katika Kijiji cha Mloka kilichopo Kata ya Mwaseni wilayani Rufiji mkoani Pwani,… Read More
0 comments:
Post a Comment