Facebook

Saturday 28 February 2015

Di Maria ajuta kujiunga na Man United


Mchezaji nyota ambaye pia ni kiungo wa kati wa Manchester United Angel Di Maria amesema kuwa alifanya makosa kujiunga na Kilabu ya Manchester United msimu uliopita.
Raia huyo wa Argentina amejaribu kuendana na maisha ya ligi ya Uingereza na majuto yake yataongeza uvumi kwamba anapanga kuondoka katika kilabi hiyo miwshoni mwa msimu huu.

Mwandishi wa Uhispania Manolete Esteban anadai kwamba mchezaji huyo wa zamani wa kilabu ya Real Madrid ambaye amekosolewa kwa uchezaji wake amewaambia marafiki zake kwamba anajuta kuondoka katika kilabu ya Real Madrid.
Esteban aliiambia runinga ya Uhispania katika kipindi cha La Goleada kwamba Di maria alikiri kwa rafikiye katika kilabu ya Real Madrid kuwa anajuta kujiunga na Manchester United.

SOURCE:BBC SPORTS

0 comments:

Post a Comment