Facebook

Friday 27 February 2015

Diamond Platnumz na A.Y waingia 10 bora katika chati za muziki Afrika.

Muziki wa Tanzania upo mahali pazuri kwa sasa. AY, Diamond Platnumz na wasanii wengine wanaiwakilisha vyema nchi yetu kimataifa.


Diamond Platnumz na Ambwene Yessayah 'AY' wakamata #1 kwenye Top 10 za muziki wa Afrika za Trace International na Soundcity

Wasanii hao wamekamata nafasi za kwanza wiki hii kwenye top ten za chart za muziki wa Afrika katika vituo vikubwa viwili vya runinga.

Diamond Platnumz amekamata nafasi ya kwanza kwenye African Top 10 ya Trace International na wimbo wake Ntampata Wapi.

Naye AY amekamata nafasi ya kwanza kwenye chart ya Africa Rox Countdown ya Soundcity kwa wimbo wa ‘Touch Me’ aliowashirikisha Sean Kingston na Ms Triniti.

0 comments:

Post a Comment