Facebook

Sunday 22 February 2015

UCHAMBUZI MECHI ZA LEO JUMAPILI LIGI KUU UINGEREZA n HISPANIA NA Mr.CHOI {KWA TAARIFA YAKO}

SOUTHAMPTON vs LIVERPOOL 19:15         
     Baada ya kuondoka kwa kocha Mauricio Pochettino na kutimkia Tottenham kisha kuuzwa kwa R.Lambert, Adam Lallana, Dejan Lovren na Shaw wengi walitaraji kuiona Soton ikiwa miongoni mwa timu zitakazo fanya vibaya msimu huu.

     Lakini pia hata msimu ulivyo anza na vijana hawa wa Koeman kufanya vyema bado maneno yakasikika ni nguvu za soda na watawaachia wenye nafasi zao ila mpaka sasa mambo ni tofauti kwani mpaka sasa kuna asilimia kubwa kwa wao kucheza michuano ya Uefa.
     Itakuwa pale St Mary’s Stadium ambapo wata pambana na Liverpool huku chagizo la mchezo ni urejeo wa Lalana ,Lambert pale St Mary's lakini pia baada ya jana Man United kupoteza dhidi ya Swansea itakuwa nafasi kwao kufanya vyema na kuwatoa Arsenal nafasi ya tatu.
    Morgan Schneiderlin Matt Targett na  Shane Long watarejea baada ya majeraha lakini watawakosa Toby Alderweireld, Jay Rodriguez, Emmanuel Mayuka na Ryan Bertrand, ngoja tusubiri kina Mane mbele ya Škrtel.

    Liverpool walio nafasi ya saba kwa pointi 42 ambao wanatafuta nafasi ya kuwa nne za juu hivi sasa wanacheza vyema huku wakichagizwa na uwepo wa Sturridge pia Raheem Sterling anaweza anza katika mchezo kumbuka amekuwa na mchezo mzuri pindi akikutana na Soton Gerrard hatokuwepo kutokana na majeraha lakini safu nzima ya ushambuliaji iko fiti dhidi ya Soton
   Michezo mitano iliyopita kwa timu zote Soton,W-2,L-2,D-1 kwa upande wa Liver,W-4,D-1.

   NB:: The Reds mpaka sasa wamefunga penati 101 katika ligi kuu zaidi ya timu nyingine yoyote.

-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------

 TOTTENHAM vs WEST HAM 15:00  
    Pale katika dimba la White Hart Lane vijana wa Mauricio Pochettino watapambana na vijana wa Big Sam mzee wa kutafuna kiboko ya timu kubwa.
   Mshambuliaji hatari Kane, Ryan Mason and Mousa Dembele wanataraji kuanza hii leo baada ya kupumzishwa katika mchezo wa Europa ligi dhidi ya Fiorentina walitoka sare ya 1-1.
     Pasipo kuwa na majeruhi Spurs walio nafasi ya 6  na pointi 43 watahitaji kushinda ilikupata matumaini ya kucheza Uefa huku katika michezo mitani iliyopita wameshinda mara-2,D-2,L-1.
    Bilashaka mshambuliaji KANE ambaye katika michezo 10 amefanikiwa kufunga goli 11 atakuwa ni mwiba kwa safu ya ulinzi ya West Ham.
     Kwa upande wa West Ham watachagizwa na urejeo wa Winston Reid na James Collins huku wakiwa nafasi ya 8 point 38 katika michezo mitano wakishinda mchezo 1,D-2,L-2.
  Kikubwa Big Sam anatafuta nafasi ya kucheza Europa hivyo siku ya leo atahitaji ushindi ilikusogeza ndoto zake, Morgan Amalfitano amefungiwa hatokuwepo huku wakimkosa  Andy Carroll msimu wote uliobakia.
   Tutaraji mchezo wa ushindani sana kutokana na uchezaji wa timu zote hasa W.ham ambao wamekuwa na kila mbinu ndani ya uwanja katika michezo miwili iliyopita ya timu hizi kulikuwa na kadi nyekundu tatu.
  Spurs ndo timu iliyo ruhusu penati nyingi mpaka sasa katika ligi penati 7 huku West Ham ndiyo timu iliyofunga magoli mengi ya kichwa 14 mpaka sasa.
  
   NB::
     Tottenham imepitisha kuanza kujenga Uwanja mpya wa White Hart Lane ambao utagharimu kitita cha pauni milioni 400.Uwanja huo utakuwa na uwezo wa kuchukua watazamani 56,000 walioketi. Unatarajiwa kuwa umekamilika na kuanza kutumika katika msimu wa 2018-19.

----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------

ELCHE vs REAL MADRID
    Vijana wa kitongoji cha ,Elche katika jiji la Valencia wanao ongozwa na Fran Escribá watakuwa katika uwanja wa nyumbani pale Martínez Valero kuwakabiri Real Madrid.
   Elche ambayo ipo nafasi ya 17 wakiwa na pointi 23 wataingia katika mchezo huu kwa kumbukumbu ya kufungwa 5-1 katika mchezo uliofanyika S.Bernabeu huku pia ikiwa ni miongoni mwa timu zenye safu mbovu ya ulinzi inayo ongozwa na Tyton; Albacar, Lomban, Roco, Suarez wakiwa wameruhusu goli 42 mpaka sasa.
    Safu ya ushambuliaji inayo ongozwa na Mbrazil  Jonathas mwenye goli 9 ndo jicho kwa vijana hawa wa Escribá huku mchezaji anaye fuata kwa wingi wa magoli ni kiungo Victor mwenye goli 3. Katika michezo mitano iliyopita wameshinda 3 na kupoteza michezo 2 .

    Vinara wa La-Liga Real Madrid wenye pointi 57 watahitaji kushinda mchezo huu ilikufikisha pointi 60 na kuwaacha Barca waliopoteza jana kwa tofauti ya pointi 4.
   Bado watawakosa Fabio Coentrao,Sami Khedira,James Rodriguez,Sergio Ramos na Luka Modriç. Lakini wacheza kama Silva ,Illarramendi,Isco na wengineo watajaza nafasi kama ilivyo kuwa katika mchezo wa Uefa dhidi ya Schalke-04.
    Katika michezo 5 Real Madrid wameshinda michezo 4 na kupoteza 1 ambao ulikuwa ule wa A.madrid.
     BBC ambayo tangu mwaka uanze haijafanya vyema mbele ya MSN ya Barca pengine kutokana na ubovu wa safu ya ulinzi ya Elche wanaweza fanya vyema leo huku Cristian Ronaldo akihitaji kuongeza utofauti wa idadi ya magoli dhidi ya Messi kwani anagoli 28 na mpinzani wake anagoli 26.


-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------

Endelea kutembelea www.bantutz.com kwa uchambuzi makini katika masuala mbalimbali hususan michezo.

---------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------

 Imeandaliwa na................
                                               CHOIKANGA
                                             Choikangta.ckt@gmail.com
                                               WhatsApp -0765 691418

0 comments:

Post a Comment