Rais Kikwete leo amekutana na mwanamuziki Diamond Platinumz na mshindi wa shindano la Big Brother Africa Idris Sultan na juwapongeza kwa ushindi walioupata recently huko Afrika Kusini.

JK amempongeza Diamond kwa kutwaa tuzo tatu za muziki za Channel O huku akimpongezza pia Idris kushinda BBA bila kufanya mambo machafu mjengoni.


Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo toka kwa msanii Naseeb Abdul “Diamond” wakati akimuonesha moja ya tuzo kati ya tuzo tano za muziki za kimataifa alizoshinda mwaka huu, Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumanne Desemba 23, 2014. kulia ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni Katika Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Profesa Hermas Mwansoko.



Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na msanii Naseeb Abdul “Diamond” baada ya kumkaribisha na kumpongeza kwa kushinda tuzo tano za muziki za kimataifa mwaka huu, Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumanne Desemba 23, 2014. Kulia ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni Katika Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Profesa Hermas Mwansoko, na kushoto ni katibu wa Bodi ya filamu Tanzania Bi. Joyce Fissoo